• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MERU YAZINDUA KAMPENI YA UTOAJI CHANJO YA POLIO KWA WATOTO WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 5

Imewekwa: May 18th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Wilayani Arumeru imezindua rasmi kampeni ya siku nne kuanzia tarehe 18 hadi 21 Mei 2022 ya chanjo ya matone ya polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 .


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya  Meru Mwl.Zainabu Makwinya amesema kampeni hiyo ya utoaji chanjo ya polio itafanyika nyumba kwa nyumba na kuhimiza kila  mzazi/mlezi kuhakikisha watoto wanapata chanjo hiyo muhimu .


Aidha, Mwl.Makwinya amesema kampeni  ya chanjo ya Polio ni ya Kitaifa na inalenga kuongeza kinga mwili kwa watoto chini ya umri wa miaka 5 ili kuzuia maambukizi ya kirusi cha Polio, ikizingatiwa kirusi hicho kiliripotiwa  kuwepo nchi jirani ya Malawi.


Aidha Mwl.Makwinya amewashukuru wadau waliochangia kufanikisha kampeni hiyo kwa kutoa magari na amewaagiza wataalum kuimarisha usimamizi wa utoaji huduma za chanjo kwa kipindi chote cha kampeni hiyo.


Mganga Mkuu Wilaya Dkt.Maneno Focus amesema chanjo ya Polio  ni muhimu sana  kwani ugonjwa wa Polio  unaosababishwa na kirusi ambacho huambukizwa kwa kula au kunywa kitu kilichochafuliwa  na kinyesi chenye vimelea  hauna tiba.


Miongoni mwa wazazi walio  hudhuria uzinduzi huo wamehimiza kila mzazi kuona umuhimu wa chanjo hiyo, Izack Pallangyo ametoa wito kwa wazazi  wa kiume kuwa mstari wa mbele kuhakikisha watoto wanapata chanjo hiyo "kinga ni bora ikizingatiwa, Polio haina tiba"amehimiza Ndg.Pallangyo


Naye Zenice Kiriho ambaye ni mama wa mtoto wa kwanza kupewa chanjo  wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo ameishukuru Serikali kuhakikisha chanjo ya polio inapatikana na kurahisisha utoaji wake ambapo mbali na kutolewa kwenye vituo vya tiba itatolewa nyumba kwa nyumba.


Uzinduzi huo wa Kampeni ya Chanjo ya Polio katika Halmadhauri ya Wilaya ya Meru umefanyika katika kituo cha Afya Usa-River ambayo  inalenga kuwafikia watoto 39,649 katika halmashauri ya wilaya ya Meru.


 _Muhimu Mtoto asiyepata chanjo ni hatari kwa maisha yake na kwa jamii inayomzunguka mwani anaweza kuambukizwa au kuwaambukiza wengine._

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa