• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MERU YAZINDUA MIONGOZO YA ELIMU,WALIMU KUWA NA UZALENDO MKUBWA KUWASAIDIA WANAFUNZI

Imewekwa: September 30th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Wilayani Arumeru yazindua  miongozo mitatu   ya usimamizi wa elimu nchini, iliyotolewa na serikali kupitia wizara ya elimu inayolenga kuimarisha utoaji wa elimu bora. miongozo hiyo ni  Mkakati wa  kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimumsingi ,Changamoto katika uboreshaji wa elimu ya msingi na Uteuzi wa Viongozi wa Elimu katika mamlaka za serikali za mitaa ,  

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru wakati wa hafla ya uzinduzi  iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Elimu Maalum Patandi,  Bw Said Mzava ambaye pia ni Afisa Tarafa, tarafa ya Poli amesema Serikali ya awamu ya Sita chini  ya  Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuongeza uwekezaji katika  sekta za Elimumsingi na Sekondari ili kuhakikisha watoto wote wa kitanzania  wakiwemo wenye mahitaji maalum wanapata elimu bora  katika mazingira rafiki.

Mzava amesema Serikali  kupitia Wizara ya Elimu imeandaa miongozo hiyo  ili  kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimumsingi na Sekondari ,kutatua changamoto katika uboreshaji wa elimu pamoja na  kuwa na viongozi watakaoleta tija kwenye sekta ya Elimu ambapo ametoa  wito kwa Walimu kutekeleza wajibu wao wa kufundisha kwa weledi na uzalendo mkubwa ili kuwasaidia walengwa ambao ni wanafunzi  

Vilevile  Mzava amehimiza kila mhusika kuzingatia miongozo hiyo ambayo utekelezaji wake umeanza ikiwa ni pamoja na uandikishaji wa darasa la awali na la kwanza unaoanza mwezi Oktoba na kukamilika kabla ya kufunguliwa shule Januari 2023.

Mwl.Marcus Nazi ambaye amemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru amesema Serikali imetumia gharama kuandaa miongozo hiyo yenye tija kwa wanafunzi wakiwemo wa  Darasa la Kwanza na la pili kumudu stadi za KKK (kusoma,kuhesabu na kuandika) hivyo walimu hawana budi kuitekeleza miongozo hiyo.

Kwa upande wake Emmy Mfuru Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri hiyo amesema Miongozo hiyo inatija kubwa kwenye kuboresha Elimu kwa kubaini changamoto pamoja na kutoa utatuzi wa changamoto hizo .

Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari wameishukuru Serikali kwa kuanda miongozo hiyo yenye mikakati mahususi ya kuhakikisha kila  mtoto wa kitanzania anapata elimu bora "Tunaishukuru Serikali kwani hata sisi wenye mahitaji maalumu ni wanufaika wa miongozo hii"amesema Hollyness mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Patandi Maalum

Aidha, hafla hiyo ya uzinduzi wa Miongozo ya elimu imewajumuisha  Maafisa toka Idara za Elimu Msingi na Sekondari,Maafisa Elimu Kata ,Watendaji wa Kata ,Wanafunzi wa Shule za msingi na  Sekondari na  wadau wengine wa elimu akiwemo Mkuu wa Chuo Patandi, Katibu CWT Wilaya ya Arumeru, Mthibiti Ubora wa Shule,Katibu TSC ambapo Maafisa elimu Kata na Watendaji Kata wamekabidhiwa miongozo hiyo.

✍️ *Awamu ya Sita na Uimarishaji,Uboreshaji Sekta ya Elimu*



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa