Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John Mongela ameridhishwa na mradi wa ujenzi wa Vyumba vinne vya Madarasa katika Shule ya Sekondari ya Kikwe Wilayani Arumeru, Halmashauri ya Meru wenye thamani ya Milioni 51.3.
Hayo yamejiri wakati wa ziara yake ya siku Moja Wilayani Arumeru ya ukaguzi wa Miradi itakayowekewa, kaguliwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru ambapo ameupongeza uongozi wa Wilaya na Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa miradi na Wananchi kwa kushiriki kikamilifu katika kuchangia na nguvu kazi.
Aidha, katika mradi huo mchango wa Wananchi ni shilingi milioni 19.1, Wahisani shilingi milioni 8.6, Halmashauri shilingi milioni 22.4 na Serikali Kuu imechangia shilingi milioni Moja.
Pia.katika kikao cha kufahamiana na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri za Wilaya ya Arusha na Meru, Mhe .Mongela amewataka Watumishi wa Umma kutekeleza wajibu wao kwa weledi ili kuwaletea Wananchi maendeleo "kila mmoja atumie taaluma yake katika kuchangia maendeleo " amehimiza Mongela.
Mhe. Mongela amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanazingatia maslai ya watumishi ikiwa ni agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan"hakuna haki bila wajibu kila mtumishi atekeleze wajibu wake"amehimiza Mongela.
Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa alitembelea miradi ya ujenzi wa Vyumba vitatu (3) vya Madarasa katika Shule ya Sekondari Kikwe, Matumizi ya TEHAMA katika Shule ya Sekondari Mlangarini na mradi wa maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe.Jerry Muro akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wakati wa kikao na watumishi Wilayani humo
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John Mongela akizungumza na Viongozi na Wakuu wa Idara na Vitengo Wilayani Arumeru katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa