• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MKURUGENZI MERU AFANYA ZIARA KATIKA ZAHANATI NA VITUO VYA AFYA .

Imewekwa: December 29th, 2023

Na Annamaria Makweba

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Mwl. Zainabu J. Makwinya ametembelea miradi ya Zahanati na Vituo vya Afya katika Halmashauri hiyo kwa lengo la kukagua ujenzi wa miradi ya kuboresha huduma za Afya na mazingira pamoja na kusikiliza kero za watumishi na wananchi katika maeneo hayo.

Katika ziara hiyo iliyohusisha Mradi wa jengo la jengo la Mama na Mtoto pamoja na Mradi wa kuboresha huduma za Afya na Mazingira katika Zahanati ya Mulala Kata ya Songoro, Zahanati ya Maji ya Chai na Kituo cha Afya Mareu Kata ya Kikatiti, Mkurugenzi Makwinya ametoa maelekezo kwa Waganga wafawidhi wa Zahanati na Vituo vya Afya kuhakikisha wanatengeneza mpango wa maendeleo ili kuleta tija katika Jamii.

" Mnatakiwa kuwa na Mpango wa maendeleo ambao utawawezesha kupanga shughuli zenu ikiwa ni pamoja na kutenga maeneo ya kuendeleza maeneo haya ya kutolea huduma. " Alisema Makwinya.

Miradi ya kuboresha huduma za Afya na Mazingira iliyokaguli ni pamoja na Shimo la kutupa Kondo, Kichomea, shimo la kutupa majivu, Choo, Stendi ya tenki yenye stoo chini pamoja na kinawia mikono. Ambapo miradi hii ipo katika hatua tofauti za ukamilishaji.

Mbali na kukagua Miradi hiyo, Mwl. Makwinya amesikiliza kero na changamoto mbalimbali za watumishi katika Kata hizo, ikiwa ni pamoja kutopanda daraja ya Mshahara, kutolipwa malimbikizo ya Mshahara pamoja na kutolipwa fedha za uhamisho.

Mwl. Makwinya ametoa maelekezo kwa Waganga Wafawidhi kukusanya taarifa za watumishi wenye madai na kuziwasilisha ofisini kwake ili aweze kuzishughulikia.

Katika ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji alifuatana na baadhi ya wataalam kutoka Halmashauri ikiwa ni sehemu ya kutoa maelekezo ya moja kwa moja kwa muhusika katika kutatua changamoto hizo.









Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa