• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MKURUGENZI MERU AHIMIZA UAMINIFU NA UADILIFU UANDIKISHAJI VYETI VYA KUZALIWA.

Imewekwa: May 9th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel Mkongo amewataka Waandikishaji Wasaidizi wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5, kufanya zoezi Hilo kwa Uaminifu, Uadilifu , Uzalendo na kuwa na dhamira  thabiti .

Mkongo amesema hayo wakati akifunga mafunzo  kwa waandikishaji hao Wasaidizi yaliyofanyika kwa siku 3 katika ukumbi wa chuo Cha Mshikamano. Mafunzo hayo yamejumuisha waandikishaji toka Kata  26 na Vituo 53 vya kutolea huduma za afya.

Mkongo amewapongeza kwa kuteuliwa  kushiriki katika utekelezaji wa zoezi  hilo nyeti na la kihistoria ambapo amewaasa kuwa makini ili kufikia lengo kusudiwa la kutoa vyeti vya kuzaliwa  kwa watoto 31,000. "umakini ni muhimu katika zoezi hili ili kuwafikia walengwa ambao ni watoto wa Kitanzania "amehimiza Mkongo.

Aidha, Mkongo ametoa Wito kwa Viongozi wa Vijiji na Vitongoji kuwahimiza Wananchi wenye watoto wa umri chini ya miaka mitano kujitokeza  kuwaandikisha.

Bi. Matha  ambaye ni miongoni mwa waandikishaji wasaidizi ameipongeza Serikali kwa kusogeza karibu na Wananchi zoezi la utoaji vyeti kwa watoto bila gharama na  kwa muda mfupi baada ya kujiandikisha.

Zoezi la utoaji vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka 5 litaanza rasmi tarehe 11Mei 2021 katika Kata zote 26 za Halmashauri ya Wilaya ya Meru pamoja na Vituo 52 vya huduma za afya ambapo  vyeti vya kuzaliwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 vitatolewa mara tu baada ya mtoto kuandikishwa katika kituo cha uandikishaji .

Ikumbukwe mzazi/mlezi anapaswa kufika katika kituo cha uandikishaji akiwa na  tangazo la kizazi au Kadi ya cliniki  ya mtoto ikiwa na majina matatu ya wazazi au cheti cha ubatizo.

Ndg.Emmanuel Mkongo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo .

Restituta Mvungi, Mratibu wa zoezi la uandikishaji vyeti vya kuzaliwa kwa  watoto chini ya maika 5 akizungumza wakati wa mafunzo.

Wawili kushoto, ni waandikishaji wasaidizi wa vyeti vya kuzaliwa na kulia ni mratibu wa zoezi hilo pamoja na wawezeshaji toka RITA na Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Waandikishaji wasaidizi vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka 5 wakati wa mafunzo.


Waandikishaji wasaidizi vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka 5 wakati wa mafunzo.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa