Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya amewataka wakuu wa Idara ya Elimu sekondari na Elimu Msingi pamoja na kamati ya ufuatiliaji miradi ya lipa kutokana na matokeo EP4R kuhakikisha miradi ya vyumba 12 vya Madarasa ,mabweni 3 na ujenzi wa vyoo 6 vya muundo wa SWASH vyenye matundu 12 inakamilika ifikapo tarehe 30 Septemba 2021.
Mwl.Makwinya amehimiza ni muhimu kwa wataalam kusimamia miradi kwa karibu na ufanisi mkubwa ili miradi hiyo iwe na tija ikiwa azma ya Serikali kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia.
Aidha,Mwezi April 2021 Serikali ilitoa zaidi ya Milioni 460 kwaajili ya ujenzi wa Miradi ya vyumba vya Madarasa 6 katika Shule za Sekondari , Madarasa 6 katika Shule za Msingi ,mabweni 3 shule za Sekondari ,vyoo 2 katika Shule za Sekondari na Vyoo 4 Shule za Msingi ambapo fedha hizo zilishindwa kutumika kutokana na changamoto ya ukosefu wa kifungu cha malipo ambayo kwa sasa imetatuliwa.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa