Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango akiwa na Viongozi wengine ikiwa ni pamoja na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabenki Tanzania (TBA), Theobald Sabi, Gavana wa Benki Kuu Tanzania, Emmanuel Tutuba, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Kaganda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John VK. Mongella, Katika Mkutano wa 21 wa Taasisi za Fedha, unaofanyika kwenye Kituo cha Mikutano ya Kimataifa Arusha (AICC) Ukumbi wa Simba jijini Arusha leo 7 Machi, 2024.
Mkutano huo wa siku mbili, ulioandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania kwa kushirikiana Benki na Jumuiya ya Umoja wa Mabenki huku mada kuu ikiwa ni kuimarisha ustahimilivu wa Sekta ya Fedha Nyakati za Changamoto za Kiuchumi.