• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AHIMIZA MIRADI KUKAMILIKA KWA WAKATI ILI KUWA NA TIJA KUSUDIWA

Imewekwa: October 24th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John Mongela amesema Serikali ya awamu ya sita  imeendelea kuleta fedha nyingi za maendeleo katika Halmashauri  7 za Mkoa huo ambapo amehimiza miradi kukamilika kwa wakati ili kuwa na tija iliyokusudiwa " Serikali inafanya jitihada kubwa kuwaletea wananchi wake  maendeleo kwa kutoa   fedha za miradi hivyo kamilisheni miradi kwa wakati na kwa ubora  "amehimiza Mhe.Mongela

Mhe.Mongela amesema hayo wakati   akikagua  ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa  katika shule   ya msingi  Kikwe iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Meru , Wilayani Arumeru ambapo Serikali imetatua changamoto ya uhaba na uchakavu  wa vyumba vya madarasa  kwa kutoa milioni 60 kwaajili ya ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa  katika shule hiyo ilijengwa toka mwaka 1974.

Mhe.Mongela ameupongeza uongozi wa Wilaya na  Halmashauri kwa Ushirikiano mzuri na wadau wa maendeleo ambapo mwekezaji RIJKZWAAAN QSEM alichangia  milioni 163 katika ukamilishaji wa Zahanati ya Maksoro ambayo  imekamilika kwa milioni 180 ikiwa ni pamoja na mchango wa wananchi na inatarajiwa kuhudumia watu 600 wa kijiji cha Maksoro na Vijiji vya Jirani.

Kipekee Mhe.Mongela amemshukuru Mhe.Rais. Samia Suluhu Hassan kwa kuamsha ari ya ukamilishaji wa  ujenzi wa Zahanati ya Kikatiti uliosimama   kwa takribani  miaka  tisa toka  kuanza kujengwa mwaka 2013 ambapo Oktoba 2021 Mhe.Rais Samia  wakati akisalimiana na wananchi wa Kikatiti alichangia  Milioni  10 za ukamilishaji wa Zahanati hiyo na kuchochea Halmashauri kuchangia Milioni 10 ,Mbunge kupitia mfuko wa Jimbo Milioni 5 na shirika  la CTSI milioni  128.

Vilevile Mongela amesema Serikali imejikita kuwaletea wananchi wake maendeleo katika sekta ya Elimu, Afya, Maji , Barabara nk ambapo ameelekeza kutekeleza miradi kwa taratibu na ubora sambamba na kutumia njia shirikishi .

Wakizungumza  kwa nyakati tofauti wananchi wa Kikwe  wameishukuru Serikali kutoa milioni 60 za ujenzi wa madarasa matatu ambapo Mkuu wa Mkoa ameongoza uchangiaji wa mifuko 380 ya Saruji kwa ajili ya  ujenzi wa madarasa mengine"Hii shule imejengwa inakaribia miaka 50 toka imejengwa madarasa ni machache na mengine yamezeka hivyo Serikali imetupa milioni 60 ya madarasa matatu na   Mkuu wetu wa Mkoa kutuwezesha kupata mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madara mengine  tunashukuru sana "amesema Joel Mbise mkazi wa Kikwe

Katika ziara hiyo Mhe .Mkuu wa Mkoa akiambatana na Viongozi wa Chama na Serikali kuanzia ngazi ya Mkoa alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya Amsha na Mradi wa  Usambazaji Maji Patandi.

Baadhi ya picha za tukio

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John Mongela (mwenye kofia), Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango (wa lwanza kulia) Mkurigenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya  na Mkurugenzi wa shirika  la CTSI Bw.Kim

Muonekano wa Zahanati ya Kikatiti

Muonekano wa Mbele wa Zahanati ya Kikatiti

Kinamama wa Kikatiti wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wakati wa Ziara.

Ukagunzi wa tenki la kuhifadhia maji katika mradi wa usambazaji maji Patandi

Ukamilishaki wa vyumba viwili vya madarasa Shule ya Msingi Samaria.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa