• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MLO BORA NI ULE WA KUZINGATIA VIRUTUBISHO NA SIYO KUJAZA TUMBO - AFISA LISHE MERU.

Imewekwa: October 18th, 2024

Afisa Lishe Halmashauri ya Wilaya ya Meru Bi. Asia Ijumaa amewataka wataalam kuendelea kutoa elimu kwa Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru kuhakikisha wanafunzi shuleni wanapata Chakula bora na chenye virutubisho ili kuwasaidia watoto kuwa na lishe bora.


Afisa Lishe amesema hayo katika kikao cha Kamati ya Lishe kilichofanyika Leo tarehe  18 Oktoba, 2024  cha kujadili taarifa za Lishe kwa kipindi cha robo ya Kwanza Julai - Septemba 2024 kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Afisa Lishe ameeleza kuwa mlo kamili ni ule unaozingatia Makundi 6 ya vyakula kwa siku, ambapo Makundi hayo ni kundi la Nafaka, Mizizi na Ndizi, Mbogamboga, Matunda, Kundi la asili ya wanyama, Jamii ya Mikunde pamoja na Mafuta yanayotokana na mimea.

Katika Kikao hicho, Divisheni za Elimu Msingi na Sekondari, Divisheni ya Afya, kilimo, Mifugo na Uvuvi pamoja na Maendeleo ya Jamii wamewasilisha taarifa na kujadili changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika maeneo yao hasa katika Divisheni ya Kilimo kuhusu mazao ya Mbogamboga na matumizi ya viwatilifu.

Afisa Kilimo Ally Isimbula ameeleza kuwa changamoto hiyo wameshaanza kuifanyia kazi na wamejipanga kutoa elimu kwa wakulima ili kuzingatia matumizi sahihi ya viwatilifu na kulinda afya za walaji wa mbogamboga kwa wananchi wa Meru na Maeneo mengine.

Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl. Zainabu Makwinya, Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Flora Msilu amewataka wataalam wanaohusika na masuala ya lishe wahakikishe wanashikiri katika vikao vya WDC na vikao vya wazazi ili kuendelea kutoa elimu kwa wazazi na jamii kuhusu masuala ya Lishe.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa