Moto wazuka kwenye Hostel ya Mwaraad Hostel iliyopo Usa-River Leganga ,janga hilo limetokea leo majira ya saa 5:00 na uharibifu wa mali za wanafunzi wanaoishi katika Hostel hiyo ambao ni wanafunzi wa chuo kikuu cha Tumaini Makumira kuombewa hifadhi ya Malazi katika shule iliyopo Jirani kwa siku kadha.
Akizungumza na wanafunzi hao Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru Timotheo Mzava amewapa pole wanafunzi hao na kumshukuru mungu kwani katika tukio hili hakuna aliyedhurika pia amewataka ambao vyeti vyao vimeunguzwa na Moto huo kwenda kituo cha polisi na kukata taarifa ya upotevu ( Loss report)
Mwangalizi wa Hostel hiyo Amina Hassan amesema ”moshi ulivuma toka chumba kimojawapo kilichokuwa kimefungwa nilipofungua moshi ukatapaka kwenye vyumba vingine “
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru Christopher J. Kazeri amesema Halmashauri imepokea tukio hilo kwa masikitiko na pia itatoa msaada wa awali kwa wanafunzi hao wanne (04) ambao vitu vyao vimeteketea kwa kuwapa kila mmoja Fedha kiasi cha Shilingi 250,000/-.
Naye Rahel Elisha ameishukuru Halmashauri hiyo na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru kwa msaada wa hifadhi ya malazi na fedha kwa ambao vitu vyao vimeteketea.
Kamanda wa zimamoto Wilaya ya Arumeru Inspector Alhaj Kimaro amesema baada ya uchunguzi imebainika chanzo cha moto huo ni jiko la gesi lililokuwa linatumika.
Baadhi ya wanafunzi wanaoishi katika Hostel ya Mwaraad wakisikiliza maelekezo ya viongozi wa Serikali
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa