• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI MERU DC MWL. MAKWINYA AMEJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

Imewekwa: October 11th, 2024

Msimamizi wa Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa  Mwaka 2024 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl. Zainabu J. Makwinya amefanya zoezi la kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura la uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa katika Kituo cha Nganana kijiji cha Nambala, Kata ya Kikwe katika Halmashauri hiyo.

Aidha, Mwl. Zainabu ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura na kuwataka watumishi wanaoishi maeneo mengine tofauti na vituo vyao vya Kazi  kwenda kujiandikisha kwenye vituo vyao mahali wanapoishi.

Hata hivyo, Makwinya ameeleza kuwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kuna vituo vya kujiandikisha na kupiga kura 338 na  zoezi hili linaanza saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni.  Pia, ameeleza wahusika ni wale walitimiza umri wa miaka 18 na kuendelea na kwa wale wanaogombea nafasi  ya uongozi ni miaka 21 na kuendelea.

Katika Zoezi hilo Mwananchi wa Kijiji cha Nambala Mathew Mtinange ameeleza kuwa zoezi hilo linafanyika kwa muda mfupi na ameshukuru amekuta waandikishaji wapo kituoni.

" Zoezi ni Zuri nimejiandikisha kwa wakati na sijatumia muda mrefu hivyo niwashauri wananchi wenzangu kujitokeza kwani ndio njia pekee ya kupata viongozi tunaowataka. " Amesema Mathew.

Kiongozi wa Kanisa la  IEC la Bishop Eliudi Issangya Kata ya Kikwe kijiji cha Nambala Mch. Simon Kaaya ameeleza kuwa zoezi hilo ni zuri na litawafanya kuchagua viongozi waliochaguliwa na Mungu na wanadamu pia.

"Uchaguzi wa Viongozi ulianzia kwenye Bibilia wakati wa Mussa hivyo ni wajibu wetu kujiandikisha ili kuweza kuchagua viongozi watakaotuongoza" amesema Mch. Kaaya.

Kwa upande wa Vijana, Rajabu Ramadhani ambaye naye amejitokeza kujiandikisha amewataka vijana kuwa wazalendo na kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la Wapiga Kura.

"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa