• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

NAIBU WAZIRI AAGIZA KUKAMATWA KWA VIONGOZI WANNE WA BODI YA MAKILENGA.

Imewekwa: August 23rd, 2019

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Juma  Aweso , ameagiza jeshi la Polisi Wilaya ya Arumeru kuwashikilia na kuwaweka chini ya ulinzi  viongozi watatu wa  bodi ya  Maji MAKILENGA  Halmashauri ya Meru,Wilayani Arumeru kwa tuhuma  za kufanya ubadhirifu kwenye Mradi huo.

Aweso ametoa agizo hilo baada ya kubaini uwepo wa ubadhirifu wa fedha za mradi huo licha ya makusanyo  ya fedha zinazotokana na uchangiaji wa huduma ya maji kufika  kiasi cha milioni tano (5) kila mwezi bodi imebakiwa na kiasi kisichozidi milioni moja na nusu tu,  “Haiwezekani asilimia kubwa ya mradi unatumia vyanzo vya mtiririko matumizi yake kuwa makubwa kiasi cha kumaliza fedha zote za miaka minne”amehoji Aweso.

Waliokamatwa kwa tuhuma za kuhujumu mradi huo ni pamoja na mwenyekiti wa Bodi Godhope Chales,Mhasibu wa Mradi Bi.Warialanga Pallangyo,pamoja na fundi bomba wa mradi huyo anayetambulika kwa jina la Kaaya.Meneja wa Mradi huo Orest Manyanga amewekwa chini ya ulinzi kwa kuonesha utovu wa nidhamu wakati wa kikao cha Naibu waziri na wajumbe wa bodi ya MAKILENGA.

Aidha Aweso ameridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa Maji Kiiji cha Kingori wenye thamani  ya Shilingi bilion 1.5 sambamba na kumpongeza mkandarasi kwa utendaji mzuri chini ya usamizi wa Uongozi wa Wilaya hiyo.

Haya yamejiri wakati wa ziara ya Naibu huyo Wilayani Arumeru iliyolenga kutembelea na kukagua Miradi ya Maji ili kuweza kutambua na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazokwamisha utekelezaji wa Miradi ya maji kwa kuzingatia utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi imeelekeza mpaka kufikia 2025 upatikanaji wa maji vijijini kuwa asilimia 85 na mjini 95.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru akieleza namna Wilaya hiyo inavyosimamia utekelezaji wa Miradi ili wananchi waweze kunufaika.

Mhe.Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki John Pallangyo akiishukuru Serikali kusikia kilio alichowasilisha Bungeni  cha wananchi Wameru kuhusu maswala ya Maji kilichopelekea Naibu waziri wa Maji kufanya ziara Wilayani hapo ili kutatua changamoto hiyo.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru,Nelson Mafie ameipongeza Serikali kwa utatuzi wa changamoto za wananchi  ambapo imeunda chombo cha wakala wa maji vijijini na Mjini (RUWASA)."huu ndio Mwarubaini wa changamoto za ya maji "amesisitiza Mafie.

Wananchi wamempongeza Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro  kwa kutumia fedha zake kugharamia kumsafirisha  Mzee Senyaeli Mbise Maarufu kama  Lemali, ambaye ni fundi mwenye uelewa wa mradi wa Maji MAKILENGA kurudi kuendelea na kazi hiyo baada ya fundi aliyekuwepo kuwa kikwazo kwenye utendaji.

Wajumbe wabodi ya MAKILENGA,viongozi na wanachi na wataalamu wakifuatilia kikao

viongozi na wanachi na wataalamu wakifuatilia kikao

Viongozi na wananchi wa Kata ya Kingori wakifuatilia kikao.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa