• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

NMB WAUNGA MKONO MCHANGO WA MHE.RAIS SAMIA, UKAMILISHAJI ZAHANATI YA KIKATITI

Imewekwa: November 11th, 2022

Benki ya NMB yakabidhi vifaa tiba kwa zahanati ya Kikatiti ikiwa ni kuunga mkono mwamko  wa ukamilishaji wa zahanati hiyo uliofanywa na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan ambapo alichangia milioni 10 za ukamilishaji wa zahanati hiyo wakati  akisalimiana na  wananchi wa Kikatiti Oktoba  2021.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa tiba hivyo Meneja wa Benki ya NMB  kanda ya Kaskazini Bwn.Dismas Prosper amesema  benki hiyo inaunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita katika kuwaletea wananchi maendeleo ambapo imetoa kitanda cha kujifungulia kinamama  ,kitanda cha wagonjwa godoro, mzani wa kuwapima uzito  wagonjwa, mizani mbili ya kupimia wtoto wanapozaliwa ,stendi za dripu  katika zahanti ya  kikatiti na katika sekta ya elimu benki hiyo imetoa bati 130 kwa shule ya Sekondari Umoja King'ori  hivyo jumla ya michango hiyo ni Shilingi Milioni saba.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru  Mhandisi Richard Ruyango ameipongeza Benki ya NMB kuunga mkono juhudi za Serikali za uboreshaji wa huduma za afya sambamba na miundombinu katika sekta ya elimu ambapo ameendelea kuikaribisha Benki hiyo kuendelea kushirikiana na Serikali kuwaletea  maendeleo wananchi "leo tumeshuhudia wananchi hawa wa Kikatiti wakituma salamu za shukrani kwa Mhe .Rai , tunaipongeza  NMB kuunga mkono hamasa hii ya Mhe.Rais"amesema mhe Ruyango

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya ameishukuri Benki ya NMB ikiwa ni mdau wa pili kuunga mkono ukamilishaji wa zahanati ya Kikatiti baada ya Shirila la  Cross Talent Share International (CTSI)  kuchangia milioni 135.38 hadi sasa katika ukamilishaji wa zahanati hiyo.

Makwinya amesema baada ya Mhe.Rais kuchangia Milioni kumi za ukamilishaji wa zahanati ya kikatiti, hamasa ilianza na  Halmashauri ilichangia milioni 10 na Mbunge kupitia mfuko wa jimbo alichangia Milioni 5 ambapo mwamko huo umeendelea kwa wadu wa CTSI na NMB.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe. Jeremia Kishili ameishukuru benki ya  NMB kuitikia  hamasa ya  ukamilishaji wa zahanati ya Kikatiti aliofanya Mhe.Samia Suluhu Hassan , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" Zahanati hii ilisimama takribani  miaka  tisa ikiwa boma, lakini Mhe. Rais alipoweka mkono wake hamasa imekua kubwa na  wananchi watanufaika na huduma " ameeleza Mhe.Kishili

Wananchi wa Kijiji cha Kikatiti wamemshukuru Mhe. Rais kuamsha ukamilishaji wa zahanati yao kwani kupitia mchango wake Halmashauri na  Wadau wamechangia, pia Serekali imeleta  wataalumu  watatu  katika zahanati hiyo "Tunamshukuru Mhe. Rais, tunaishukuru NMB   kwani vifaa hivi vitatumika katika utoaji wa huduma na kutuondolea  kero kubwa na gharama za kupata  huduma za afya katika umbali mrefu" amesema Mwenyekiti wa Kijiji cha Kikatiti

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru  Mhandisi Richard Ruyango akizungumza katika hafla ya NMB kukabidhi vifaa tiba.

Meneja wa Benki ya NMB  kanda ya  Kaskazini Bwn.Dismas Prosper akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa tiba.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe. Jeremia Kishili akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba.

Mwl.Zainabu Makwinya akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa