Na Annamaria Makweba
Halmashauri ya Wilaya ya Meru imefanya kikao cha kujadili Rasimu ya Mpango wa Bajeti ya Awali ya Lishe kwa mwaka wa Fedha 2024/2025.
Mratibu wa Lishe Mkoa wa Arusha Doto Milembe amewasilisha Rasimu hiyo na kueleza kuwa Rasimu ya mpango wa Bajeti ya Awali ya Lishe kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 ni shilingi 138,075,000.00.
Aidha, Mratibu wa MTUHA Mkoa wa Arusha, Agripina Tarimo ametoa mafunzo ya mfumo wa taarifa za uendeshaji wa huduma za ( MTUHA) kwa wajumbe wa Kamati ya Lishe.
Mratibu wa MTUHA Ameeleza kuwa, MTUHA ni mfumo wa kukusanya, kutunza, kuchambua na kutafsiri taarifa za Afya na zile zinazohusiana na Afya kutoka katika Vituo vya kutolea huduma, lengo hasa ikiwa ni kupata takwimu na kutoa maamuzi yanayohusiana na utendaji wa shughuli katika sekta husika.
Vilevile Mfamasia wa Mkoa Thobias Ngonyani ameelezea mpango mkakati wa usimamizi wa bidhaa za Afya katika Vituo vya kutolea huduma na taratibu za uthibiti na usimamizi wa bidhaa mbalimbali kutoka Bohari ya Madawa(MSD).
Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Arumeru, Loveness Mlawa ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuelekeza kufanyika kwa Mafunzo haya kwani hii italeta tija na kusaidia kuboresha lishe katika jamii.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa