• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

RUWASA YASIKILIZA CHANGAMOTO ZA CBWSOs ARUMERU.

Imewekwa: July 4th, 2024

fungua hapa kupata video,☝️Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini  RUWASA Wilaya ya Arumeru imefanya Mkutano Mkuu wa nusu mwaka wa Pili kwa Vyombo vya watoa huduma ya maji ngazi ya Jamii (CBWSOs) Wilaya ya Arumeru na kusikiliza changamoto mbalimbali za vyombo vya watumia maji.

Mkutano huo umefanyika leo katika ukumbi wa St. Carolus Tengeru na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kama vile Waheshimiwa Madiwani,Watendaji wa Kata, Wataalamu wa Halmashauri, Maafisa Tarafa, Viongozi wa Dini, Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Wataalamu wa Bonde ( Pangani na Kati)Meneja wa Maabara ya Maji pamoja na viongozi wa Vyombo vya watoa huduma ya maji ngazi ya jamii Arumeru.

Kati ya Changamoto zilizowasilishwa katika Mkutano huo ni uharibifu wa miundombinu, Taasisi kutolipa bili za maji, kupasuka kwa mabomba, baadhi ya viongozi kuhamasisha jamii isichangie huduma za maji, malipo ya uendeshaji wa miradi kuchelewa na kupelekea ufuatiliaji wa vyombo hivyo kuwa mgumu.

Meneja wa RUWASA Arumeru Mhandisi Shabib Waziri ameeleza kuwa Mkutano huo ndio Nuru kwa namna gani miradi au skimu za maji zitakavyoendeshwa na kusimamiwa ili kutoa Matunda.

" Hapa ndio sehemu sahihi ya kujadili changamoto zetu za vyombo vya watoa huduma za maji na sisi kama RUWASA tutoe changamoto zetu, tusisubiri afike kiongozi mkubwa ndio tuanze kutoa changamoto wakati tungeweza kuzifanyia kazi wenyewe" amesema Waziri.

Pia, ameeleza kuwa hawategemei ikitokea Ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo wakutane na malalamiko kuwa shule haina maji au Zahanati haina maji wakati maombi yao ya kuomba huduma hiyo hayakuwasilishwa RUWASA.

Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Kaganda, Afisa Tarafa ya Poli Ndg. Jiliki Milinga amewataka Viongozi mbalimbali walioshiriki katika Mkutano Mkuu wa Wilaya kwa vyombo vya watoa huduma ya maji ngazi ya jamii kwenda kutoa elimu kwa wananchi umuhimu wa maji na kuchangia huduma ya maji ili vyanzo vya maji viweze kutunzwa na kutumika kwa vizazi vijavyo .

Milinga ameeleza kuwa adhma ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuhakikisha tunamtua Mama Ndoo Kichwani na Serikali imeongeza fedha kutoka Bilioni 1 hadi Bilioni 6 ya utekelezaji wa miradi ya maji kuhakikisha adhma hiyo inatimia.

Kati ya Vyombo vya watumia maji viliyoshiriki Mkutano huo kwa Halmashauri ya Meru ni pamoja KIWANGO, MAKIMAKA, AMSHA, KIMASAKINA, MAKILENGA, NGUNGYESA na vingine.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa