• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

SERIKALI YAFUTA SHAMBA LA VALESKA WILAYANI ARUMERU .

Imewekwa: June 1st, 2021

Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi, amesema Serikali imefuta Shamba la Valeska lenye ekari 4087  kwa manufaa ya Halmashauri ya Wilaya ya  Meru.

Aidha, Mhe.Lukuvi ameeleza kuwa Serikali imeelekeza kuwa  jumla ya ekari 1500 zitagawia kwa Vijiji 3 vya Kwaugoro, Maroroni na Valeska vinavyopakana na Shamba kwa mgawanyo wa ekari 500 kila Kijiji. Pia Serikali imeelekeza ekari 1028 zitatumika kwaajili ya kilimo na ekari 1659 zitatumika kwaajili  ya makazi na biashara.

Mhe. Lukuvi amewataka Madiwani wa Halmashauri hiyo  kusimamia mgawanyo wa Shamba hilo kwa maslahi mapana ya Halmashauri.

Aidha, katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru,  Mhe.Lukuvi   ametoa tamko la kufuta  waraka namba moja  wa Ardhi uliotolewa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuwa unawanyima haki Madiwani kushiriki katika upangaji wa Ardhi kwenye maeneo yao. "wataalam wawashauri Madiwani ili wafanye maamuzi sahihi na si kuwapangia " amehimiza Mhe Lukuvi

Aidha, Mhe.Lukuvi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuwatumia Wataalamu wa Ardhi na kuwawezesha Kutekeleza majukumu yao.

Mhe.Jerry Muro, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ameishukuru  Serikali na kuahidi kutekeleza maagizo ya Mhe .Waziri ambapo utekelezaji umeanza kwa kuwa na kikao na Madiwani mara baada ya ziara ya Mhe. Waziri Lukuvi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Mhe.Jeremia Kishili ametoa wito kwa Madiwani kushirikiana   kupanga Shamba hilo sambamba na kuwaelimisha Wananchi kwani ugawaji wa Shamba hilo unalenga kupunguza changamoto za uhaba wa Ardhi na kuongeza mapato ya Halmashauri kwa maendeleo ya Wananchi.

Akishukuru kwa biaba ya Waheshimiwa Madiwani Mhe.Shari Pallangyo ameishukuru Serikali kwa kufuta Shamba hilo na kueleza kuwa wapo tayari kufanyia kazi Maelekezo yaliyotolewa na Serikali.

Ikumbukwe kuwa kabla Serikali kutoa Maamuzi hayo, Shamba hilo lilikuwa linamilikiwa na Chama cha Ushirika(ACU).

Mhe. William Lukuvi,  Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru.kulia kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe.Jeremia Kishili, Kushoto kwa Waziri ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe.Jerry Muro, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg.Emmanuel Mkongo  na wakwanza kulia ni Karibu Tawala Wilaya ya Arumeru Mwl.James Mchembe

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru akizungumza wakati wa Mkutano wa Waziri Lukuvi na Madiwani wa Halmashauri hiyo.

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa Mkutano.

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati Mkutano

Wataalam Ngazi ya Mkoa,Wilaya na Wananchi wakati wa Mkutano

Watumishi wa Halmashauri wakati wa Mkutano.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa