• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

SERIKALI YATOA SIKU 7 KUREJESHWA KWA MASHINE KATIKA KITUO CHA AFYA MOMELA ILI WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA.

Imewekwa: February 13th, 2020

Naibu waziri wizara ya afya Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt.Faustine Ndugulile alipotembelea Kituo cha afya Momela kilichopo  Halmashauri ya Meru ,Wilayani Arumeru kufuatia mgogoro uliopelekea kuondolewa kwa baadhi ya huduma kutokana na Wafadhili  wa kituo hicho Shirika la Africa Amini Alama kuondoa baadhi ya mashine ,ameliagiza shirika hilo kurejesha mashine zote zilizokuwa zikitumika katika kituo hicho ndani ya siku 7 ili wananchi waendelee kupata huduma zote zilizokuwa zinatolewa hapo awali.

Naibu waziri ametoa agizo hilo kwenye mkutano wa hadhara ya wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki ,ikiwa ni baada ya kikao kati ya uongozi wa Wilaya ya Arumeru,Uongozi wa Halmashauri na wafadhili wa Shirika la Africa Amini Alama ambapo alieleza kuwa serikali yaTanzania ipo tayari kufanya ushirikiano na wadau wa afya kwa kuzingatia Sheria,kanuni ,taratibu na miongozo ya sekta hiyo.

Aidha, kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kilipo kituo hicho Dkt. Maneno Focus, Kituo cha afya Momela kimesajiliwa ni mali ya umma na kina watumishi wa Serikali na hupokea dawa toka Bohari ya dawa pamoja na fedha za wahisani mbalimbali zikiwemo fedha za Busket fund.

Aidha, taarifa imeonesha mwaka 2009 kijiji cha Olkung'wado kilitenga ekari 10 za ardhi kwaajili ya ujenzi wa zahanati iliyokamilika 2010 na kukabidhiwa Serikalini ambapo ilisajiliwa mwaka 2012 kama zahanati ya kijiji cha Okungwado momela na mwaka 2013 Serikali iliingia makubaliano ya uboreshaji Zahanati hiyo na wafadhili wa Africa Amini Alama. Mnamo mwaka 2015 Zahanati hiyo ilipandishwa hadhi kuwa kituo cha afya.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Ndg.Emmanuel Mkongo katika kikao alisema Halmashauri hiyo ilishindwa kuridhia ombi la wafadhilli la kubadilisha Kituo cha afya Momela ambacho ni cha Umma (public) kuwa Hospitali ya binafsi ya wahisani (Charitable private Hospital) kwakuwa ni kinyume cha Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo    za uendeshaji na usimamizi wa Vituo vya kutolea huduma.

Mkongo alisema Halmashauri inathamini mchango wa wafadhili wa Africa Amini Alama na ilitaka  kumaliza changamoto zilizojitokeza kwa kushirikisha Mamlaka mbalimbali za Serikali kwa mujibu wa     Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo   za uendeshaji  na usimamizi wa Vituo vya kutolea huduma. 

Mhe.Ndugulile baada ya kikao ametoa mwelekeo wa Serikali kuwa, kituo hicho kitabaki kuwa mali ya umma na kitakapokidhi vigezo kitapandishwa hadhi kuwa Hospitali ya umma na siyo ya binafsi kama wafadhili walivyoomba, ”hatuwezi kutoa kituo cha umma kwa mtu binafsi”amesisitiza Ndugulile.

Kwa upande wa Wafadhili  Christine Wallner ambaye ni Rais wa Shirika la Afrika Amini Alama ameishukuru serikali kwa kutatua mgogoro huo na kueleza kuwa  shirika lipo tayari kuendelea kufadhili kituo hicho sambamba na kutekeleza agizo la kurejesha mashine maeneo husika. Pia ameiomba Serikali kuharakisha maandalizi ya makubaliano ya kuboresha utoaji huduma Kituoni hapo.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amemuomba Mhe. Naibu waziri kupokea ombi la Wananchi la kukipandisha hadhi kituo hicho cha afya kuwa Hospitali ili kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za afya, pia ametoa wito kwa wananchi kutokuwa sehemu ya kuchochea migogoro .

Mhe. Mbunge wa Jimbo la Arumeru mashariki, Dkt.John D. Pallangyo ameishukuru Serikali namna inavyowathamini wananchi wake kwa kufanyia kazi ombi lao alilowasilisha la kuomba utatuzi huduma kusitishwa katika kituo hicho cha afya.

Nao Wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki wameiomba Serikali kuharakisha mpango wa kuandaa makubaliano ya uendeshaji wa kituo hicho pamoja na kukipandisha hadhi kuwa Hospitali.

Naibu waziri wizara ya afya Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt.Faustine Ndugulile akizungumza kwenye mkutano wa hadhara ya wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki.

Naibu waziri wizara ya afya Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt.Faustine Ndugulile akizungumza kwenye kikao cha Uongozi wa Wilaya ya Arumeru,uongozi wa Halmashauri ya Meru na Wafadhili.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru , Jerry Muro akizungumza wakati wa  mkutano wa Mhe.Naibu waziri na wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki.

Wakwanza kushoto mwa Mhe .Naibu Waziri Dkt.Faustine Ndugulile ni, Mganga Mkuu Mkoa wa Arusha Dkt. Wedson Sichalwe na  pembeni yake  ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Ndg.Emmanuel J. Mkongo.

Mhe. Mbunge wa Jimbo la Arumeru mashariki, Dkt.John  D. Pallangyo akizungumza wakati wa Mkutano na wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki.

wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki wakati wa Mkutano.

Christine Wallner ambaye ni Rais  wa Shirika la Afrika amini alama akizungumza wakati wa  mkutano wa Mhe.Naibu waziri na wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki.

wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki wakati wa Mkutano

Cornelia Wallner ambaye ni Mkurugenzi   wa Shirika la Afrika amini alama akizungumza wakati wa  mkutano wa Mhe.Naibu waziri na wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki.

wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki wakati wa Mkutano.

wananchi wa Kijiji cha Olkung'wado Kata ya Ngarenanyuki wakifurahia maamuzi ya Serikali.

Ndg. Mollel akizungumza wakati wa Mkutano

Naibu waziri na viongozi alioambatana nao akitembela kitou cha Afya Momela 

Dkt. Veronica Gisambo akitoa maelezo kwa Naibu waziri wizara ya afya Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt.Faustine Ndugulile akitembela kituo cha Afya Momela .

aliyeshika Karatasi Nyeupe ni,Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Dkt. Maneno Focus,

Naibu waziri akimsalimu mmoja wa wagonjwa alipotembelea  kituo cha Afya Momela .


Naibu waziri na viongozi alioambatana nao akitembela kitou cha Afya Momela 


Naibu waziri Dkt.Faustine Ndugulile akikagua vifaa  akitembela kitou cha Afya Momela 




Naibu waziri Dkt.Faustine Ndugulile akitembela kituo cha Afya Momela .




Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa