• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2019 SHULE YA SEKONDARI KISIMIRI YAWA KINARA.

Imewekwa: July 12th, 2019

Shule ya Sekondari Kisimiri ambayo ni shule ya Serikali ya Kata iliyopo Halmashauri ya Meru ,Wilayani Arumeru Mkoani Arusha ndio shule ya Sekondari bora kati ya shule 594 Nchini Tanzania.

Ubora wa Kisimiri umetokana matokeo ya kidato cha sita mwaka huu 2019, jumla ya  wanafunzi 60 waliofanya Mtihani huo kati yao 58 wamepata ufaulu wa daraja la kwanza na wanafunzi wawili tu ndio waliopata daraja la pili.

Mbali na ufaulu wa madaraja kwa wanafunzi, shule hiyo imeongoza kitaifa kwa kushika nafasi ya kwanza katika masomo 3 ambayo ni  Kingereza, Histori na Kemia. Pia katika somo la Fizikia na Hisabati imeshika nafasi ya tatu kitaifa.

Jumla ya wanafunzi 4 wa shule hiyo wameweza  kuingia kwenye kumi bora kitaifa wakiongozwa na Mwanafunzi wa kwanza kitaifa kwenye masomo ya Sayansi Hermani Mugisha sambamba na kutoa wanafunzi bora 2 wautafiti wa kisayansi.

Mkuu wa Shule hiyo Mwl.Valentine Tarimo amesema Serikali imechangia kwa kiasi kikubwa shule hiyo kufanya vizuri kwa kugharamia kwa asilimia 100 chakula cha wanafunzi hao wa kidato cha tano na sita ambapo zaidi ya milion 72 hutumika kila mwaka pamoja na kuboresha miundombinu kupitia mradi wa P4R shule ilipewa zaidi ya milioni 500 za  ujenzi wa mabweni 2,madarasa 8 vyoo vya matundu 10 na miradi hii yote imekamilika.

Mwl Tarimo amesema uongozi wa shule hiyo umejiwekea mkakati uitwao (Ufaulu mzuri) unaolenga walimu kufundisha kwa malengo na kusimamia malengo yao kwa wanafunzi hao kupata matokeo mazuri ambao umekua na mafanikio makubwakwani  kwa kipindi cha  miaka 3 mfululuzo ufaulu wa kidato cha sita  umekua ukiongezeka, ambapo mwaka 2017  shule hiyo ilishika nafasi  ya 3 kitaifa, 2018 ikawa ya 2 na mwaka huu imekua ya kwanza.

Mwl Tarimo amesema ufundishaji mzuri wa walimu,  utayari wa wanafunzi,usimamizi mzuri wa bodi ya Shule,Ushirikiano kutoka Halmashauri ,Mahusiano Mazuri ya Jamii inayozunguka shule, mchango wa wadau wa Elimu (friends of Kisimiri) vimepelekea kupata matokeo hayo.

Aidha Tarimo mbali na shukuru Serikali kwa kuajiri walimu 3 wa masomo ya sayansi ameomba kuongezewa Walimu wa masomo hayo kwa kuwa bado kuna uhitaji.

Shule hiyo ya Kisimiri yenye walimu 55 wanafunzi 1000 na watumishi wasio walimu iliyopo umbali wa Km 37 toka makao makuu ya Halmashauri ya Meru , kwa sasa nui gumzo Nchini Tanzania.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa