• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WATAKAO KUWA KIKWAZO KWENYE UTOAJI WA CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA MLANGO WA UZAZI KUWAJIBISHWA.

Imewekwa: April 25th, 2018

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Idd Kimanta amesema hatua kali za kisheria zitachikuliwa dhidi ya mtu yoyote atakaye kuwa kikwazo kwa namna yoyote kwenye zoezi la utoaji chanjo ya kinga ya Saratani ya shingo ya mlango wa kizazi inayotolewa kwa watoto wenye umri wa kuanzia miaka 9 hadi 14 kwani chanjo hiyo ni juhudi  ya Serikali kutokomeza saratani hiyo kwa kizazi kijacho.

Mhe. Kimanta amesema hayo wakati wa uzinduzi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Meru wa chanjo  ya Kinga ya saratani ya shingo ya kizazi (HPV)uliofanyika katika Hospitali ya Wilaya Tengeru  ambapo ametoa agizo kwa maafisa elimu ,watendaji wa Kata na Vijiji na viongozi wote kwenye Halmashauri hiyo kuhakikisha watoto walengwa kwenye maeneo yao wanapata chanjo hiyo.

Naye mganga mkuu kwenye Halmashauri hiyo Dkt.Cosmas Kilasara ameeleza kuwa kati ya wanawake elfu 5,892 waliofanyiwa uchunguzi wa saratani ya shingo ya mlango wa kizazi  mia 319 kati yao walibainika kuwa na maambukizi ya awali na mia 119 walikuwa wamepata mashambulizi makubwa ya saratani hiyo hivyo walipewa rufaa kwenda hospitali ya juu zaidi pia ametoa wito kwa wanawake kufanya uchunguzi mara kwa mara wa Saratani hiyo kwani huwa rahisi kutibika inapokuwa kwenye hatua za awali.

Dkt. Kilasara ameenda mbali zaidi kwa kueleza Ugonjwa huo wa Saratani ya shingo ya mlango wa uzazi (HPV)  hutokana na mabadiliko ya ukuwaji wa seli kwenye mwili wa mwanamke  ambayo huathiri misuli na viungo vingine  na visababishi vya saratani hiyo ni pamoja na kufanya mapenzi kwenye umri mdogo,kuwa na wapenzi wengi,ndoa za mitara,kuzaa watoto wengi pamoja na uvutaji wa sigara.

Mratibu wa chanjo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Jonathan Mollel ametoa wito kwa wasichana kutoshiriki tendo la ndoa wakiwa na umri mdogo pia amewasihi wazazi kushiriki kikamilifu kuhakikisha watoto wao wenye umri husika wanapata chanjo hiyo ya kinga ya saratani ya shingo ya kizazi ,sambamba na wanawake kuwa na utamaduni wa kufanya uchunguzi wa afya zao mara kwa mara.

Mmoja wa wasichana waliopata chanjo hiyo (jina limehifadhiwa) ameishukuru Serikali kwa kumtamini mwanamke kwani mwanamke anapokua salama familia huimarika.

PICHA ZA TUKIO.


Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Idd Kimanta akizungumza wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kinga ya saratani ya mlango wa kizazi.

Mganga mkuu kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Meru akizungumza wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kinga ya saratani ya ahingo la mlango wa kizazi.


Mmoja ya wasichana waliopata chanjo ya kinga ya saratani ya shingo la kizazi.

Wasichana walipata chanjo ya Saratani ta shingo la mlango wa kizazia  wakiwa kwenye uzinduzi.

Wasichana walipata chanjo ya Saratani ta shingo la mlango wa kizazia  wakiwa kwenye uzinduzi.

Wasichana walipata chanjo ya Saratani ta shingo la mlango wa kizazia  wakiwa kwenye uzinduzi.

Kinamama waliowaleta watoto wak kupata chanjo mbalimbali ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya chanjo

Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Wilaya Tengeru na wazazi wakiwa kwenye uzinduzi.

Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Wilaya Tengeru na wazazi wakiwa kwenye uzinduzi

Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Wilaya Tengeru na wazazi wakiwa kwenye uzinduzi
Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Wilaya Tengeru na wazazi wakiwa kwenye uzinduzi

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa