• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Uzinduzi wa huduma ya upasuaji kwa mama wajawazito katika kituo cha afya Usa - River

Imewekwa: September 17th, 2019

 Witness Ayo ambaye ni mkazi wa Leguruki ameweka rekodi ya uzinduzi wa huduma ya upasuaji katika Kituo cha Afya Usa –River kilichopo Halmashauri  ya Wilaya ya Meru baada ya kujifungua mtoto kwa kufanyiwa upasuaji kituoni hapo.

Mganga Mfawidhi wa  kituo hicho, Dkt. Nuruel Kitomari amesema zoezi hilo la upasuaji limeenda vizuri na kuishukuru Serikali kwa kutenga Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya uboreshaji wa Kituo hicho kwa kujenga majengo mapya likiwemo jengo la upasuaji.

Dkt. Kitomari amesema kuzinduliwa kwa huduma hiyo kutawapunguzia wananchi gharama kwa kuwa huduma hiyo ni bure katika vituo vya afya vya Serikali ukilingalinganisha na vituo vingine pia   kupunguza msongamano katika Hospitali ya Wilaya. Aidha, uwepo wa Kituo hicho utasaidia mama wajawazito katika maeneo ya Usa River na maeneo jirani kupata huduma za uzazi hususani upasuaji kwa urahisi zaidi.

Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dkt.Focus Maneno amesema Serikali imelenga kuboresha huduma za afya ambapo upatikanaji wa dawa katika Halmashauri hiyo ni asilimia 98%, pia katika  kuondoa vifo vitokanavyo na uzazi  Serikali imesogeza huduma hizo karibu na wananchi ambapo  huduma ya upasuaji kwa Mama wajawazito inapatikana katika vituo vya afya vitatu vya Halmashauri hiyo ambavyo ni Usa – River, Kituo cha Afya Mbuguni na Kituo cha afya Momela.

Akizungumza na Mwandishi wetu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Ndg. Emmanuel Mkongo amesema uboreshaji wa Sekta ya Afya ni kipaumbele cha  Serikali ya awamu ya tano, Serikali katika  mwaka wa fedha 2017/2018 ilitoa Shilingi milioni 500 kwaajili ya ujenzi na uboreshaji wa Kituo cha Afya Usa -River hususani ujenzi wa majengo  mapya ambayo ni jengo la maabara, nyumba ya mtumishi, jengo la upasuaji, wodi ya mama na mtoto, chumba cha kuhifadhia maiti, kichomea taka  pamoja na kufanya ukarabati wa majengo yaliyokuwepo ambayo ni Jengo la kuwahudumia wagonjwa wa nje  (OPD), jengo la duka la dawa ambalo awali lilitumika kama kama jengo la Maabara, Jengo lenye  pande mbili likitumika kama wodi ya wanawake na wanaume  .      

BAADHI YA PICHA.

                                                            

Madaktari na wataalam wa afya wakati wa zoezi la upasuaji kituo cha Afya Usa - river.

Mashine ya dawa za usingizi katika chumba cha upasuaji kituo cha Afya Usa river.

Taa maalumu  katika chumba cha upasuaji kituo cha Afya Usa river.

Chombo cha kutakasia vifaa vya  upasuaji kituo cha Afya Usa river.

Kitanda maalumu cha kubeba Wagonjwa wa upasuaji katika kituo cha Afya Usa - River

Muonekano wa ndani wa jengo la upasuaji katika kituo cha Afya Usa - River.

Muonekano wa nje wa Jengo la upasuaji kituo cha Afya Usa -River.

Jengo la Wodi ya  Mama na Mtoto katika kituo cha Afya Usa - River.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa