• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WANANCHI WAITIKIA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA ARUMERU MASHARIKI

Imewekwa: July 20th, 2019

Afisa mwandikishaji Jimbo la Arumeru Mashariki Ndg.Emmannuel Mkongo akizungumza na mwandishi wetu,amesema mwitikio wa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la mpiga kura jimbo humo upo vizuri  kwani Katika Kata alizotembelea Akheri,Kwarisambu, Poli wananchi wanajitokeza kwa wingi haswa vijana waliotimiza miaka 18 wanaojiandikisha kwa mara ya kwanza, pia katika Kata hizo mwitikio ni mkubwa zaidi maeneo yenye mikusanyiko ya watu unaotokana na shughuli za kibiashara tofauti na maeneo ya pembezoni ambapo mwitikio ni mdogo.

Mkongo amesema hakuna changamoto iliyojitokeza ikaahiri zoezi  hilo hadi sasa kwani baadhi ya Mashine za Bvr  zilizo kuwa na itilafu na shindwa kuchapa  vitambulisho ilitatuliwa na wataalamu wa TEHAMA  "Nilipopita kukagua zoezi hili la uandikishaji  Kituo cha Kupigia chuo cha Mifugo Tengeru LITA  nilikuta BVR KIT haifanyi kazi  na kwa sasa wataalam wa TEHAMA mameshatatua na wananchi wanapata huduma"ameeleza Mkongo.

Mkongo ametoa rai kwa  Wananchi kuhifadhi vizuri vitambulisho vyao vya  Mpiga Kura  kwani wengi wao wanaokwenda kuboresha taarifa zao  imeoneka vitambulisho vyao vya awali kuharibika (vunjika) kutokana na kuvikali vikiwa mifukoni nk, "Ndugu Mwananchi Kitambulisho cha mpiga kura ni kitambulisho muhimu kwani kinakupa haki ya kikatiba ya kushiriki uchaguzi mkuu wa Rais ,Mbunge na Diwani hivyo hamna budi kuvihifadhi vizuri" amesisitiza Mkongo. 

Mkongo ametoa rai kwa wananchi ambao wanataka kurekebisha na  kuhamisha taarifa zao,kufuta taarifa zao, wanaotimiza umri wa  miaka 18 ifikapo tarehe 28 Mwezi Octoba 2019 na wenye miaka umri wa 18 ambao hawajajiandikisha kujitokeza na kujiandikisha na kupata vitambulisho vya Mpiga Kura kwani zoezi hilo litadumu kwa siku saba tu, kuanzia tarehe 18 /07/2019 hadi tarehe 24/07/2019.

PICHA ZA TUKIO

Afisa uandikishaji jimbo la Arumeru Mashariki ,ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru NDG.Emmanuel Mkongo akifuatlia utendaji wa BVR KIT Operator Ndg.Mbora Kweka ,katika kituo cha kupiga kura Mkwakirika Kata ya Poli.

Ndg.Ayob Mbise akiwa ameripoti kituo cha kupiga kura Nkwakirika kwaajili ya kujiandikisha.


Mwandishi msaidizi Ndg.Christopher Saimon akimwelewesha mama aliyefika kujiandikisha ,BVR KIT operator akimwandikisha Ndg.Ayoub Mbise.

Ndg.Ayob Mbise akitia saini yake kwenye Mashine ya BVR

Ndugu Ayob Mbise akiweka alama za vidole wakati wa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la mpiga kura.

Ndg.Ayob mbise akiweka alama za vidole wakati wa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la mpiga kura.

Zoezi la kujiandikisha likiendelea katika Kituo cha kupiga kura Poli chama cha Msingi.

Wananchi wakipata ufafanuzi katika kituo cha  kupiga kura Poli chama cha Msingi.

Afisa uandikishaji Jimbo la Arumeru Mashariki akipokea maelezo toka kwa BVR KIT operature Geturd Mkumbwa na Mwandishi msaidizi Nakaji Lukumay kituo cha kupiga kura Polli chama cha Msingi.

Afisa uandikishaji Jimbo la Arumeru Mashariki akikagua utendaji wa BVR KIT operato Ndg.David Josiah, kituo cha kupiga kura Makumira Consumer.

Zoezi la uandikishaji daftari la kudumu la mpiga kura likiendelea katika kituo cha kupigia kura Makumira Consumer.

BVR KIT , kituo cha kupiga kura Makumira Consumer, Ndg. David Josiah akimkabidhi  kitambulisho cha mpiga kura miongoni mwa wananchi waliojitokeza kuboresha taarifa zao katika daftari la mpiga kura.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa