• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WATUMISHI WA KITUO CHA AFYA USA -RIVER WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA UTABIBU KUWAHUDUMIA WAGONJWA .

Imewekwa: August 10th, 2018

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru amewataka watumishi wa Kituo cha Afya cha Usa-River, kuwahudumia wagonjwa wanaofika kituoni hapo kwa kuzingatia maadili ya utabibu yanayo sisitiza kutoa huduma Kwa viwango bora na Kwa wakati.  

Akiongea na watumishi wa kituo hicho amefafanua kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kusogeza huduma za Afya karibu na wananchi hivyo hawanabudi kuwahudumia wananchi hao Kwa huduma stahiki na Kwa wakati kama miongozo ya kitabibu inavyotaka.  "Serikali ilitoa milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa majengo  mapya kituoni hapo ambayo ni jengo la maabara,nyumba ya mtumishi, jengo la upasuaji, wodi ya mama na mtoto, chumba cha kuhifadhia maiti, kichomea taka pamoja na kufanya ukarabati wa majengo yaliyokuwepo kwa lengo la kuwapa wananchi huduma bora za afya na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

Mkurugenzi Kazeri amewaonya watumishi wa kituo hicho  ambao hutumia lugha isiyo ya staha Kwa wagonjwa pamoja  na wanaopokea  rushwa kwa wagonjwa kuacha mara moja, kwani Serikali haitawavumilia mtumishi wa namna hiyo ambaye anakwenda na kinyume cha maadili ya utabibu pamoja na azma ya serikali ya kutoa huduma bora ya Afya Kwa wananchi ,""amesema Kazeri.     


Kazeri ameongeza kuna umuhimu kwa wasimamizi wa kituo hicho kupanga utaratibu utakaowezesha vikao vya asubuhi  kutokuwa sababu ya wagonjwa kukosa huduma.

Naye Mganga mfawidhi wa kituo hicho Dkt. Aggrey Kibutu amemthibitishia Mkurugenzi huyo kutekeleza maagizo yake kwa  kutoa huduma bora Kwa wananchi Kwa kuwa wanatambua dhamira ya serikali katika kuboresha huduma ya Afya nchini.  "Kituo Chetu kina watumishi wengi wapya ambao wamehamishiwa hapa lakini tunaendelea kujipanga kwani idadi ya wagonjwa tayari imeongezeka  mara tatu katika  kituo cha Afya Usa –River , na hii ni baada ya   uboreshaji  wa miundombinu , ambapo idadi ya wagonjwa wa nje (out patient) imeongezeka kutoka wagonjwa   600  kwa mwezi hadi  wagonjwa 2000 na zaidi kwa mwezi,  hivyo tunakuahidi kuboresha utendaji kazi wetu Kwa watakao fika kupata huduma" Amesema Kibutu

Mkugenzi wa Halmashauri hiyo ametembelea kituo hicho  ikiwa  Ni Sehemu ya kuhakikisha watendaji wa Halmashauri hiyo  wanatekeleza majukumu yao na wananchi wanapata huduma bora.

PICHA ZA TUKIO.

Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri  ya Wilaya ya Meru Christopher Kazeri akizungumza na watumishi wa  wa kituo cha Afya Usa- River.

Watumishi wa  wa kituo cha Afya Usa- River wakifuatilia kwa makini mazungumzo wakati wa kikao baina yao na Mkurugenzi Kazeri.

Mganga mfawidhi wa kituo  kituo cha Afya Usa- River ,Dkt. Aggrey Kibutu akizungumza katika kikao cha Mkurugezi wa Halmashauri ya Meru na watumishi wa kituo hicho.

Watumishi wa  wa kituo cha Afya Usa- River wakifuatilia kwa makini mazungumzo wakati wa kikao baina yao na Mkurugenzi Kazeri.

Kushoto kwa Mkurugenzi Kazeri ni Mkuu wa idara ya utawala Grace Mbilinyi na kulia kwa Mkurugenzi ni Afisa utumishi Edward Chitete.

Watumishi wa  wa kituo cha Afya Usa- River wakifuatilia kwa makini mazungumzo wakati wa kikao baina yao na Mkurugenzi Kazeri.

Watumishi wa  wa kituo cha Afya Usa- River wakifuatilia kwa makini mazungumzo wakati wa kikao baina yao na Mkurugenzi Kazeri.

Watumishi wa  wa kituo cha Afya Usa- River wakifuatilia kwa makini mazungumzo wakati wa kikao baina yao na Mkurugenzi Kazeri.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa