• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAHESHIMIWA MADIWANI MERU DC WAMEFANYA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO

Imewekwa: April 30th, 2024

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Meru wamefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Kati ya miradi iliyokaguliwa ni pamoja na ukamilishaji wa vyumba 2 vya madarasa shule ya Sekondari ya King'ori iliyopo Kata ya Malula ambayo ilipatiwa fedha kutoka Serikali Kuu kwa mpango wa kuboresha Elimu ya Sekondari ( SEQUIP) kiasi cha shilingi Milioni 25 .

Aidha, Wajumbe wamekagua umaliziaji wa jengo la Zahanati ya Ngejisosia iliyopo Kata ya Malula iliyopelekewa fedha kutoka mapato ya Ndani kiasi cha shilingi Milioni 32.

Miradi mingine iliyokaguli ni ukamilishaji wa madarasa mawili katika shule ya Sekondari Kitefu na Ukarabati wa Madarasa Mawili Shule ya Msingi Nkoanekoli.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Jeremia Kishili ametoa pongezi wa Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu wa shule hizo pamoja na Zahanati kwa usimamizi mzuri wa matumizi ya fedha katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Vilevile, amesisitiza walimu kuhakikisha wanawachukulia hatua wazazi na walezi ambao hawachangii Chakula shuleni, kwani kutofanya hivyo ni kurudisha nyuma maendeleo ya taaluma ya mtoto awapo shuleni.

" Serikali imetoa fedha nyingi kuhakikisha wanafunzi wanakuwa katika mazingira bora ya kusomea, lakini tukumbuke kuwa mtoto hawezi kusoma au kumsikiliza mwalimu akiwa na njaa. Hivyo kwa wale wazazi watakaokaidi kuchangia chakula shuleni hatua zichukuliwe ili waweze kuchangia" amesema Mhe. Kishili.

Katika hatua nyingine Wajumbe hao na timu ya Menejimenti wametoa pongezi na kuchangia zaidi ya fedha sh. Laki 2 na nusu kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Nkoanekoli kwa usimamizi mzuri wa fedha shilingi Milioni 7 walizopokea kutoka mapato ya Ndani ya Halmashauri kwa ajili ya ukarabati wa madarasa mawili.

Mwenyekiti wa Halmashauri kwa niaba ya wajumbe wote amemkabidhi mwalimu mkuu fedha hizo kama mchango wa kuanzia kununua mifuko ya simenti ya kufanya ukarabati wa darasa jingine na kuahidi kutafuta fedha za kuwaongezea ili kukarabati madarasa mengine kwani shule hiyo ni kati ya shule kongwe iliyoanzishwa mwaka 1963.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa