• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAJAWAZITO WAPEWE ELIMU WAHUDHURIE KLINIKI MAPEMA - DC MKALIPA.

Imewekwa: December 27th, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Amir Mkalipa amewataka wataalamu wa Afya kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii ili kuhimiza kina mama wajawazito kuanza mapema kuhudhuria Kliniki na kujua hali zao ili kuondokana na vifo vinavyotokana na uzazi.

Mkalipa ameeleza hayo katika kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) cha Halmashauri ya Wilaya ya Meru cha kujadili taarifa kipindi cha Julai hadi Septemba 2024 kilichofanyika tarehe 27 Desemba 2024 katika Ukumbi wa shule ya Sekondari Muungano iliyopo Usariver.

" Hakikisheni elimu inatolewa kwa jamii na wazazi wote kuzingatia muda wa kuanza kliniki ili kujua hali zao za kiafya kabla ya kujifungua, wakati wa kujifunga na baada ya kujifungua kwani Vifo vingi ni kutokana na kutozingatia huduma ya Afya ya Uzazi na Mtoto." Amesema Mkalipa.

Aidha, ameeleza kuwa Halmashauri ya Meru iweke mikakati ya kuondoa vifo vya uzazi kutoka kifo 1 hadi 0 pamoja na kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka 5 kwa mwaka 2025 na hili linawezekana endapo elimu itawafikia walengwa kwa wakati.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Ndewirwa Mbise ameshiriki kikao hicho ameshauri kuwa Viongozi wa Dini na Wazee wa Mila washirikishwe katika vikao vya Afya ya Msingi ili waweze kusaidia kutoa elimu katika maeneo yao ili kina mama Wajawazito wapate elimu ya kuhudhuria Kliniki.

Pia, katika eneo la usafi wa Mazingira, Ndugu Mbise ameshauri kuwa wataalamu wafuatilie na kuhakikisha vikao vya vijiji na Kamati mbalimbali hasa Kamati ya Mazingira zikae ili kujadili masuala ya Mazingira.

Mhe. Mkalipa amesisitizia wataalamu kusimamia kwa karibu huduma zinazotolewa na mfuko wa Afya ya Jamii iliyoboreshwa (iCHF) ili wananchi kuona faida ya kujiunga na mfuko huo.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa