• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wajumbe wa baraza la Wafanyakazi Halmashauri ya Wilaya ya Meru wahimiza bajeti kuzingatia mazingira rafiki kwa Wafanyakazi.

Imewekwa: January 27th, 2020

Baraza la wafanyakazi Halmashauri ya Wilaya ya Meru lahimiza Halmashauri hiyo mbali na jitihada zilizofanyika  za kuzingatia maslahi  ya Watumishi katika maandalizi ya bajeti ya mwaka 2020/2021 kuhakikisha ina weka miundombinu rafiki kwa wafanyakazi wenye mahitaji maalum ili kuleta usawa mahala pa kazi.

Mwakilishi wa wafanyakazi  wenye ulemavu Bibi.Vicky Kimaro  amesema usawa kwa watumishi ni jambo muhimu  hivyo Halmashauri  haina budi kuboresha   miundombinu rafiki kwa wafanyakazi wenye mahitaji maalum katika vituo vya kazi haswa vilivyopo pembezoni ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi  na kuleta tija.

Akitoa mfano Bibi Vicky amesema baadhi ya Shule za Msingi na Sekondari hakuna vyoo kwa ajili ya Watumishi wenye mahitaji maalumu.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa baraza hilo  Bi.Grace Mbilinyi ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu amesema katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri itaendelea kuweka bajeti ya mahitaji mbalimbali ikiwa ni pamoja na miundombinu ya wafanyakazi wenye mahitaji maalumu.

Afisa Maendeleo ya Jamii kwenye Halmashauri hiyo Ndg.Hamson Mrema ametoa wito kwa walemavu kuchangamkia fursa ya mkopo kwa gharama nafuu unaotolewa na Halmashauri.

Mrema amesema mbali na Halmashauri hiyo kutenga bajeti kwa ajili ya mikopo kwa walemavu  ni kikundi kimoja pekee cha watu wenye mahitaji maalumu kilichojitokeza kuomba mkopo Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2018/2019 na kwa mwaka huu 2019/2020 hadi sasa ni  vikundi Vinne  pekee vimejitokeza.

Aidha Mrema amefafanua kuwa fedha za mikopo kwa gharama nafuu zinazotolewa kupitia mfuko wa Wanawake,vijana na walemavu kwa asilimia zinalenga kuwasaidia kuboresha  shughuli za kiuchumi wanazofanya  kwa kuwaongezea mtaji hivyo kigezo cha kuwa na shughuli ya kiuchumi kabla ya kupewa mkopo huzingatiwa.

Aidha viongozi  toka vyama mbalimbali vya wafanyakazi ngazi ya Mkoa na Wilaya waliweza kuipitia bajeti hiyo na kutoa maoni yao ambapo Katibu wa TUGHE Mkoa wa Arusha Ndg. Samweli Magero ametoa rai kwa Halmashauri kuhakikisha maoni ya Baraza hilo na maboresho kuhusu  maslahi ya watumishi yaliyotolewa kuzingatiwa kabla bajeti hiyo haijaenda hatua nyingine.


Mwakilishi wa walimu kutoka Shule ya Sekondari Makiba Mwl. Vistus Sylidion ameipongeza Halmashauri kwa kufuata sheria kuhakikisha wafanyakazi wanashiriki kikamilifu katika mchakato wa bajeti.

Mkutano huo maalumu wa baraza la wafanyakazi kujadili bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa Mwaka wa fedha 2020/2021 umefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa kushirikisha wafanyakazi wote kutoka Idara 14 na Vitengo 6 vya Halmashauri pamoja na viongozi kutoka vyama  vya wafanyakazi TUGHE, CWT, TALGU, TTU, RAAWU


Mwenyekiti wa Baraza ka wafanyakazi Bi.Grace Mbilinyi akizungumza.

Mwakilishi wa wafanyakazi wenye Ulemavu Wilaya ya Arumeru Bibi Vicky Kimaro akitoa maoni juu ya miundombinu rafiki.

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa Baraza.

Katibu wa CWT Mkoa wa Arusha Ndg.Felix Mnyanyi akihoji kiwango cha posho kwa watumishi.

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa Baraza.

Katibu wa TUGHE Mkoa wa Arusha Ndg. Samweli Magero akizungumza .

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa Baraza.

Katibu wa CWT Wilaya ya Arumeru akizungumza.

Katibu wa baraza la wafanyakazi Oliver Swaty na  kushoto ni katibu msaidizi Charles Mungure

Katibu wa TALGU Mkoa wa Arusha Ndg.Jonathan Ndumbaro akizungumza.

Mapitio ya  Bajeti ya Halmashauri.

Kulia ni Katibu wa RAAWU Mkoa wa Arusha akichambua bajeti 

Mapitio ya  Bajeti .

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa Baraza.


Tovuti yetu .www.merudc.go.tz


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa