• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WALIMU WA SHULE ZA MSINGI MERU WAPEWA MOTISHA,MHE.RAIS APONGEZW A

Imewekwa: June 3rd, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Meru kupitia idara ya elimu msingi  imetoa motisha kwa Walimu, Wanafunzi, Shule na Kata  zilizofanya vizuri katika mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mwaka 2021.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo ya utoaji motisha, Mkuu wa Idara ya elimu ya awali na msingi Mwl. Marcus Nazi amesema motisha hiyo ni hamasa kwa walimu,uongozi wa shule na  jamii  kushiriki kikamilifu kuhakikisha kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bora ambapo kwa shule zilizofanya vibaya zimepewa cheti cha onyo ili kuwakumbusha uwajibikaji.   "tunatambua   mchango wa walimu , kazi mnayofanya ni kubwa na sisi tupo nyuma yenu.”Amesema Mwl.Nazi

Mwl.Nazi amesema elimu ya msingi ni muhimu kwani mtihani  wa kumaliza elimu ya msingi unapima kiwango cha kumudu stadi na maarifa aliyoyapata  mwanafunzi  kwa miaka 7  hivyo ufundishaji na usimamizi mzuri huchangia kwa kiasi kikubwa kumwezesha mwanafunzi kufanya vizuri .


Katibu tawala Wilaya ya Arumeru Mwl.James Mchembe ambaye amemwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo , amepongeza walimu kwa  ufaulu mzuri ,ambapo Halmashsuri ya Wilaya ya Meru imeshika nafasi 3 Kimkoa "niwapongeze kwa matokeo haya mazuri,nitoe wito kwenu walimu tuendelee kutekeleza majukumu kwa ufanisi mkubwa kwani Mhe.Rais wetu anawajali watumishi na ameshaanza kuboresha maslahi ya watumishi"amesema Mwl.Mchembe

Mwenyekiti wa chama cha Walimu (CWT)Wilaya ya Arumeru  Isaack Kamalang'ombe amesema Serikali ya awamu ya sita kwa kipindi kifupi imeleta neema na kuongeza nuru kwa walimu na watumishi wengine ambapo   watumishi walinufaika na mserereko wa kupanda madaraja, kubadilishiwa muundo ,punguzo la kodi ,kupandisha asilimia ya kikokoto cha pensheni sambamba na maboresho mengine yaliyoridhiwa na yanayotarajiwa  kuanza  mwaka wa fedha ujao "hakuna haki bila wajibu ,wito wangu kwenu tuendelee kutekeleza wajibu wetu"amesema kalamang'ombe.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Walimu wa shule na masomo  yaliyofanya vizuri  wameishukuru  Halmashauri kwa  kutambua mchango wao na kutoa wito kwa shule zilizo fanya vibaya kuongeza juhudi kupandisha ufaulu "tunashukuru kwa motisha hii,tunaahidi kufanya vizuri zaidi "amesema  Tajieli Mbwambo ambaye ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Leganga ambayo ni miongoni mwa shule zilizopandisha ufaulu.


Dkt.Amani Sanga ambaye amwemwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru amewashukuru wadau na wote waliohusika kufanikisha hafla hiyo inayolenga kuchochea kupanda kiwango cha ufaulu Meru.


Mhe, Kaanael Ayo ambaye ni  Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu ,Afya na Maji amekabidhi vyeti vya pongezi na fedha taslimu kiasi cha shilingi laki moja kila mmoja kwa walimu 12 waliofaulisha zaidi katika masomo yao, madaftari/ counter books 5, Rimu moja ya karatasi na cheti cha pongezi kwa wanafunzi 4 waliofanya vizuri wakiwemo wa elimu maalum. Amekabidhi vyeti vya pongezi na Sukari kwa makundi ya  shule bora 10 za serikali na zisizo za serikaali zilizokuwa na watahiniwa zaidi 40,shule bora 10 za serikali na zisizo za Serikali zilizokuwa na watahiniwa chini ya 40,shule 10bora za serikali zilizokuwana  watahiniwa zaidi 40 na shule bora 10 za serikali  zilizokuwa na watahiniwa chini 40 .Katika kila kundi  shule ya kwanza imepewa kg 25 za sukari shule ya 2-3 kg 20 na Shule ya 4 hadi ya 10 zimepewa  sukuri kg 10.


Pia Mhe.Ayo amekabidhi vyeti vya  pongezi kwa Shule 10 zilizopandisha ufaulu, cheti cha pongezi kwa Kata tatu zilizopandisha ufaulu,cheti cha onyo kwa shule 10 zilizoshuka ufaulu, cheti cha onyo kwa kundila  shule 5 zilizokuwa na watainiwa zaidi ya 40 na  zilizokuwa na watainiwa chini 40,cheti cha onyo kwa Kata 3 zilizoshuka ufaulu na cheti kwa Mdau  wa The foundationi for tommorow.

Halfla ya utoaji motisha imefanyika katika ukumbi wa Shule ya  Msingi Mariado

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa