• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WANANCHI 224,499 MKOANI ARUSHA WANATARAJIWA KUANDIKWA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA KWA UCHAGUZI MKUU 2025

Imewekwa: November 29th, 2024

Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs C. M. Mwambegele na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi leo tarehe  29 Novemba, 2024 amekutana na Wadau wa Uchaguzi katika Mkutano wa Tume hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya  Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Lengo la Mkutano huo ni kuanza maandalizi ya zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mwaka 2024 kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, 2025 ambapo jumla ya wapiga kura wapya 224,499 wanatarajiwa kuandikishwa Mkoani Arusha.

Mhe. Jaji (Rufaa) Mwambegele ameeleza kuwa kwa mujibu wa Ibara ya 74(6) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ya Mwaka 1977, Tume imepewa Mamlaka ya kutekeleza majukumu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusimamia na kuratibu Uandikishaji wa Wapiga Kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano na Madiwani kwa Tanzania Bara.

Aidha, ameeleza kuwa zoezi hili lilishaanza kwa baadhi ya maeneo na Mikoa kama vile Geita, Kagera, Kigoma, Tabora, Katavi,  Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu Manyara,Dodoma,Singida na Zanzibar lakini kwa sasa Tume inafanya maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la kudumu kwa Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Mkoa wa Dodoma kwenye Halmashauri za Kondoa, Chemba na Mji wa Kondoa kuanzia tarehe 11 Desemba, 2024 hadi tarehe 17 Desemba, 2024.

Uboreshaji wa Daftari la kudumu la Wapiga kura utahusisha matumizi ya teknolojia ya Biometric Voters' Registration BVR ambao hutumika katika kumtambua mtu na kumtofautisha na mwingine kwa kuwa unahusisha uchukuaji wa alama za vidole vya mikono, picha na saini na kuhifadhiwa kwenye kanzidata ya wapiga kura.

Wadau walioshiriki katika Mkutano huo pamoja na Vyama vya Siasa vyenye Usajili, Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia, Taasisi, Makundi mbalimbali ya Vijana, Wanawake, watu wenye Ulemavu, Wahariri, Waandishi wa Habari na Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri katika Mkoa wa Arusha.

Mhe. Mwambegele katika Mkutano huo ameambatana na  Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima, R. K na Mhe. Dkt. Zakia Abubakar Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Mratibu wa Uandikishaji wa Mkoa

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa