• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WANANCHI WA KIJIJI CHA MAJI YA CHAI WATAKA MRADI MPYA WA USAMBAZAJI MAJI KUANZA KUTEKELEZWA

Imewekwa: November 14th, 2017

Wananchi wa Kijiji cha Maji ya Chai Halmashauri ya Meru wakiwa kwenye mkutano wa kijiji wamepokea Uibuaji wa Mradi Mpaya wa usambazaji Maji kijijini hapo utakao tekelezwa kwenye vitongoji 3 Maji ya Chai Center,Kimandafu na K.center na kuomba mradi huo kuanza kutekelezwa mapema kwani upatikanaji wa maji kwao umekua changamoto waliyoifananisha na kilio,

Pia wanachi hao wameridhia kuunganishwa kwenye Mamlaka ya Maji Usa -River ili kulipia huduma ya Maji itakayowawezesha kupata maji kila siku tofauti na sasa ambapo upatikanaji wa maji si wa uhakika pia ni mdogo jambo ambalo ni kero kubwa kwao,

Akieleza manufaa ya kupata huduma ya maji kupitia Mamlaka ya Mji mdogo Usa-River Meneja mwendeshaji  wa mamlaka hiyo Mhandisi Antidius Mchunguzi amesema Mamlaka hiyo itawaezesha wananchi hao kupata Huduma ya maji ya uhakika yaani kila siku, na kupunguza gharama za kununua Maji sh 500 kwa(dumu) lita20  waliyokiri kulipia ambayo ni kubwa sana ukilinganisha na itakayotozwa na mamlaka hiyo sh 6, akisistiza ulipaji nafuu wa tozo za maji kwa msemo wa "Tozo za maji sio biashara" . 

Naye Mhandisi wa Maji Happy Mrisho amesema kuwa Mradi huo unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na Serikali ya Tanzania unazingatia lengo la serikali la kutaka wananchi Kusimamia, Kuipenda na kuthamini Miradi ya Maji katika Maeneo yao hii ni kwa mujibu wa Sheria  namba 12 ya huduma ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Christopher J.Kazeri amewataka wananchi hao kuchagua wajumbe wa kamati watakao kua na uelewa mpana wa maeneo ya kijiji hicho  jamba ambalo litakua msaada kwa wataalamu wa idara ya maji wakati wa kufanya uchunguzi wa awali  wa mradi huu pia amewaasa kutokuchagua wajumbe hao kisiasa .

Akizungumza kwa niaba ya wanawake Ndeterivio S. Sumari ambaye ni mama wa familia kutoka Kitongoji cha Kimandafu ameishukuru Halmashauri ya Meru kwa Kupeleka Mradi huu utakao waondolea kinamama adha ya upatikanaji wa Huduma ya Maji ikiwa ni kupoteza muda mwingi wa kuchota maji umbali mrefu tena maji kidogo

Ndeterivio S. Sumari akizungumza kwa niaba ya wanawake kwenye Mkutano wa wanakijiji wa Maji ya Chai.

Meneja mwendeshaji wa Mamlaka ya Maji Usa-River Mhandisi Antidius Mchunguzi           



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa