• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WANANCHI WA SAMARIA WATAKIWA KUTOKUWA NA HOFU JUU YA ZOEZI LA UTAMBUZI WA MIPAKA YA UWANJA WA NDEGE KIA

Imewekwa: May 25th, 2018

Mwakilishi wa mkuu wa Wilaya ya Arumeru Timotheo Mzava ambaye pia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru amewatoa hofu wananchi wa kijiji cha Samaria kuhusiana na zoezi la kutambua  eneo la uwanja wa ndege wa  kimataifa Kilimanjaro (KIA) kwa kuweka alama.

Mzava amesema hayo kwenye mkutano wa hadhara ya wananchi hao uliolenga kufikisha ujumbe wa Serikali kuwa mnamo mwaka 1969 Serikali ilitenga eneo kwa ajili ya kiwanja cha ndege KIA na mwaka 1989 upimaji rasmi wa eneo hilo ulifanyika ambapo mwaka 2001 ilifanyika tathimini ya wananchi walioingia kwenye eneo hilo ambapo jumla ya kaya 289  zilionekana kuwa ndani ya eneo la uwanja huo wa KIA, hivyo Serikali imeamua kufanya tathimini ya kutambua  watu waliopo kwenye eneo la uwanja kwa kutambua eneo la uwanja na kuweka alama kwa lengo la kupata uhalisia na baada ya hapo itarudi kushauriana na wananchi kwa hatua nyingine.

Mzava ameenda mbali zaidi kwa kueleza kwenye Wilaya ya Arumeru jumla ya vijiji vinne baadhi ya maeneo yake yameingia kwenye uwanja ikiwemo kijiji cha Samaria ,Malula,Majengo kati  na Kaloleni hivyo amewaomba wananchi wa maeneo hayo kuwa watulivu na kutoa ushirikiano wakati wa utambuzi wa mipaka na kuweka alama kwani Serikali ni ya watu na ipo kwaajili ya watu  hawapaswi kuwa na hofu.

Wananchi wengi wameonesha kuwa na hofu na kutaka kufahamu hatma yao ikiwa maeneo yao yatakuwa kwenye eneo la uwanja wa ndege KIA na kujibiwa kuwa baada ya utambuzi wa kiwanja kufanyika na kujua nani yuko ndani ya eneo hilo na maendelezo yaalilomo Serikali itarudi kukaa nao jambo lililowatia moyo na kupungua kwa maswali.

Yonas Kimiree ambaye ni miongoni mwa wananchi ambao maeneo yao yanasadikika kuwa ndani ya eneo la uwanja wa ndege KIA amesema wananchi wanaimani na Serikali ya awamu ya tano kwa namna inavyofanya kazi hivyo hawana budi kukubali utambuzi wa eneo la uwanja kufanyika kwani wanatumai serikali itarudi kushauriana nao nini kifanyike

Nae Gadi Shami ameshukuru kwa ufafanuzi mzuri uliotolewa pia amesema wananchi hawawezi kupinga maendeleo na kuiomba serikali kuchukua maoni ya wananchi kuyafanyia kazi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Christopher Kazeri ametoa rai kwa wananchi hao kutokushirikiana na watu wenye nia ovu ambao baada ya kusikia swala la utambuzi wa eneo la uwanja wanatafuta maeneo huko.

Mwakilishi wa mkuu wa Wilaya ya Arumeru Timotheo Mzava ambaye pia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru akizungumza na wananchi wa kijiji cha Samaria

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Christopher Kazeri akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Samaria

Afisa Ardhi Mteule kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Meru ,Judas T. Mahuma akizungumza kwenye hadhara ya wananchi wa kijiji cha Samaria.

Wananchi wa Kijiji cha Samaria wakifuatilia kwa makini maelezo ya zoezi la utambuzi wa eneo la kiwanja cha ndege KIA

Wananchi wa Kijiji cha Samaria wakifuatilia kwa makini maelezo ya zoezi la utambuzi wa eneo la kiwanja cha ndege KIA

Wananchi wa Kijiji cha Samaria wakifuatilia kwa makini maelezo ya zoezi la utambuzi wa eneo la kiwanja cha ndege KIA

Mwananchi wa kijiji cha Samaria Gadi shami ameiomba Serikali kuzingatia maoni ya wananchi kwenye zoezi la utambuzi wa eneo la uwanja wa ndege KIA na hatua zitakazofuata.

Yonas Kimiree ambaye ni miongoni mwa wananchi ambao maeneo yao yanasadikika kuwa ndani ya eneo la uwanja wa ndege amesema wananchi hawawezi kupinga maendeleo hivyo wanaridhia zoezi la utambuzi wa eneo la uwanja wa ndege KIA kuendelea

Wananwake wakijiji cha Samaria wameiomba Serikali kuzingatia maoni ili hatma yao iwe ya heri.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa