• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

NAIBU WAZIRI WA AFYA,MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WAZEE NA WATOTO AONYA UKOSEFU WA DAWAA KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFY

Imewekwa: December 15th, 2017


Naibu waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto  Fautine Ndugulile awataka watumishi wa  Afya kwenye Halmashauri ya Meru kutekeleza majukumu yao kuendana na kasi ya Mhe. Raisi wa awamu ya tano John Joseph Magufuli,  hayo ameieleza timu ya uendeshaji wa huduma za afya katika Hopitali ya wilaya ya Halmahauri hiyo alipokua kwenye ziara yake ya siku moja yenye lengo la kuangalia hali ya upatikanaji wa dawa na kujiridhisha na utoaji wa uduma za afya.

Aidha Naibu waziri huyo ameipongeza Halmashauri hiyo kwa matumizi mazuri ya fedha kwani imeweza kuboreha  na kufanya upanuzi wa majengo ya wodi ya kina mama wajawazito, jengo la huduma ya Meno (Dental Unity) na jengo la utawala pongezi hizi amezito  sambamba na kufanya vizuri kwenye utoaji wa chanjo,usafi unaoridhisha kwenye Hospitali hiyo ya Wiaya na utoaji wa huduma za afya jambo ambalo amejiridhisha baada ya kutembelea maeneo kadha ya kutolea huduma kwenye hospitali hiyo na kuwahoji wagonjwa namna wanavyohudumiwa .

Naibu Waziri amesema Serikali imeongeza bajeti ya Dawa kwa asilimia 80 kutoka kiasi cha bilioni 30 hadi bilioni 261 hivyo hategemei mwananchi  kukosa dawa kwenye vituo vya kutoa huduma za Afya na kuviagiza vituo hivyo kuhakikisha vinaagiza dawa zote zinazohitajika pia  katika kudhibiti matumizi ya dawa hizo ujazaji wa fomu za huduma za dawa (BIN GARD)  ufanyike .

Katika kutatua changamoto zilizopo kwenye Idara hiyo ya Afya ameshauri ni vema kukawa namipango mikakati ya kukabiliana na vifo vya mama na mtoto,magonjwa yasiyoambukiza kwani yameshamiri kwa sasa na uzazi wa mpango ,Naibu huyo amemtaka meneja wa MSD Kanda ya Kaskazini Billy Singano, kutembelea mara kwa mara Hospitali ili kujua changamoto za upatikanaji wa dawa na kuzifanyia kazi kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma za Afya . 

Akizumngumza na  Wananchi waliokua wameudhuria matembezi shirikishi(Site walk through) yaliyofanyika kwenye kituo cha Afya Mbuguni yakifadhiliwa na shirika la Engender Health kwenye Mradi wa LAD kwa lengo la jamii hiyo kutembelea kituo hicho cha Afya na kuibua changamoto zilizopo pamoja na  kuzitatua zile zinazowezekana kwa ngazi yao ambapo wananchi hao wameweza kutatua  changamoto ya chumba cha kuhifadhia chanjo kuvuja na kutokua kwenye hali nzuri  kwa kuchangia bati 6 na mbao pamoja changamoto ya upungufu wa viti  kwa kuchangi Fedha sh 205,000 na viti 6,huku wakichukua baadhi ya changamoto zilizo baki na kuhaidi kuzifanyia kazi ikiwemo upatikanaji wa maji, Amewataka wananchi hao kua mstari  wa mbele kwenye kudhibiti matumizi mabaya ya dawa kwa kuhakikisha  wawakilishi wao waliopo kwenye bodi wanakwepo wakati wa mapokezi ya dawa.Pia amewata wananchi hao kushiriki shughulli za maeneleo ikiwemo kutat.ua changamoto ndogondogo zilizopo kwenye kituo hicho, na  kuliponeza Shirika lililoandaa matembezi haya, naye  Sebastani Macrice kutoka shirika  hilo la Engender Health  ambaye ni Afisa mradi huo wa LDA amesema matembezi hayo  shirikishi ni sehemu pia ya jamii hiyo kupata elimu juu ya huduma zinazopatikana katika kituo hicho ,elimu juu ya uzazi wa mpango pamoja na Huduma ya mama mjamzito ambaye mimba itaharibika kusafishiwa Hospitali.

Naye mganga mkuu wa Halmashauri hiyo Cosmas Kilasara ametatu changamoto ya gari la kubebea wagonjwa lililodaiwa na wananchi kama changamoto kubwa  kwakua umbali kutoka kituo hicho hadi Hospitali ya Wilaya nizaidi ya Kilometa 30 kwa kuhaidi kituo hicho kitapewa gari hilo hivi karibuni.

Sebastiani Macrice kutoka shirika la Engender Health ambaye ni Afisa Mradi wa LAD akieleza umuhimu wa matembezi shirkishi

Kushoto ni Naibu waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto  Fautine Ndugulile akisalimiana na Mganga Mkuu wa Hamashauri ya Meru Cosmas Kilasara alipowasili kwenyenye Hospitali hiyo ya Wilaya kwaajili ya ziara  ya siku moja.

Naibu waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto  Fautine Ndugulile akiwauliza kinamama waliohudhuria waliowaleta watoto wao kliniki katika kituo cha afya Usa-River  namna huduma zinavyotolewa kituoni hapo.

Kulia ni Mkurugenzi wa MSD Taifa Victoria Elangwa ,Kushoto kwake ni Meneja wa MSD kanda ya Kaskazini Billy Singano 


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa