• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wanawake 123 Wanufaika na uboreshaji wa Kituo cha Afya Usa River.

Imewekwa: January 31st, 2020

Wanawake wapatao  123  Wilayani Arumeru Mkoani Arusha wamenufaika na ujenzi na ukarabati wa Kituo cha Afya Usa –River  kilichopo  Halmashauri ya Wilaya ya Meru,ikiwa ni baada ya Serikali kutoa Milioni 500 kwaajili ya ujenzi na Ukarabati  wa Kituo Hicho.


Mganga Mfawidhi wa kituo cha Afya Usa – River,  Dkt.Hillary Mkini  amesema tangu kuzinduliwa kwa huduma ya Upasuaji kituoni hapo tarehe 17 Septemba 2019 jumla ya wagonjwa 132 wamefanyiwa upasuaji, kati yao kinamama wajawazito ni 123  na wagonjwa 9 walifanyiwa upasuaji wa kawaida .

Dkt.Mkini amesema kunaongezeko kubwa la idadi ya wagonjwa wanahudumiwa kituoni hapo ambapo kabla ya uboreshaji idadi ya wagonjwa ilikuwa wagonjwa 600  hadi 800 kwa Mwezi na Wakiongezeka sana walifika 1,200  tofauti na sasa ambapo idadi ya wagonjwa ni 2,500 hadi 3,000 kwa mwezi.

Mkini amehitimisha kwa kutoa wito kwa jamii kupata huduma katika kituo hicho na kueleza kuwa hali za wagonjwa wote waliofanyiwa upasuaji kituoni hapo  zilikuwa nzuri na wote  waliruhusiwa kwenda Majumbani .

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Ndg. Emmanuel J. Mkongo amesema uboreshaji wa Sekta ya Afya ni kipaumbele cha Serikali ya awamu ya tano kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma bora za afya katika umbali mdogo.

Mkongo ameishukuru Serikali kwa kutoa Shilingi milioni 500 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwaajili ya ujenzi na ukarabati wa Kituo cha Afya Usa -River hususani ujenzi wa majengo mapya 6 ambayo ni jengo la upasuaji, nyumba ya mtumishi, jengo la maabara, wodi ya mama na mtoto, chumba cha kuhifadhia maiti na  kichomea taka pamoja na kufanya ukarabati wa majengo 3 yaliyokuwepo ambayo ni Jengo la kuwahudumia wagonjwa wa nje (OPD), jengo la duka la dawa ambalo awali lilitumika kama kama jengo la Maabara na  Jengo wodi ya wanawake na watoto.

Naye Witness Ayo ambaye ni mkazi wa Leguruki aliyeweka rekodi ya uzinduzi wa huduma ya upasuaji katika Kituo hicho tarehe 17 Septemba 2019  ameishukuru Serikali ya awamu ya Tano kwa kuboresha sekta ya Afya kwani imeokoa maisha ya kinamama wengi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Ndg. Emmanuel J. Mkongo.


Mganga Mfawidhi wa kituo cha Afya Usa – River,  Dkt.Hillary Mkini  

Jengo la upasuaji katika kituo cha Afya Usa – River. 

Jengo la Wodi ya mama na mtoto katika kituo cha Afya Usa – River.  


 Jengo la maabara katika kituo cha Afya Usa – River.

Nyumba ya mtumishi katika kituo cha Afya Usa – River. 


Wananchi wakipata huduma katika Jengo la kuwahudumia wagonjwa wa nje (OPD)

.

Muonekano wa ndani wa jengo la upasuaji katika kituo cha Afya Usa - River.


Taa maalumu  katika chumba cha upasuaji kituo cha Afya Usa river.



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa