• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WATEJA WA NMB KUJITENGENEZEA FAIDA 12%,DC ARUMERU APONGEZA KIAPO CHA HUDUMA KWA WATEJA

Imewekwa: October 4th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi, Richard Ruyango wakati wa maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja katika  Benki ya NMB  tawi la Usa River, amepongeza Juhudi na ubunifu wa Benki ya NMB, ya  kuwa na Kiapo  cha utoaji huduma kwa usikivu na weledi mkubwa ikiwa ni pamoja na  kutunza taarifa za wateja, ambapo amehimiza  Benki hiyo kuzingatia Kiapo ilichojiwekea Ili kiwe na tija zaidi.

Meneja wa NMB tawi la Usa-River Ndg. Mitabalulo Elisha Semuguruka akisoma taarifa ya maadhimisho ya wiki ya Mteja kwa niaba ya  Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Taifa, amesema katika maadhimisho hayo Benki hiyo imezindua rasmi Kiapo cha huduma kwa wateja kikilenga utoaji wa huduma za uhakika na kuaminika, usikivu, weledi, uaminifu na kutunza taarifa za wateja kwa lengo la kutoa huduma Bora zaidi na shindanishi zenye tija kwa Benki na wateja wake.

Semeguruka amewatambua na kuwashukuru wateja wa Benki hiyo wakiwemo Watumishi wa Serikali na wasio wa Serikali, wafanyabiashara wakubwa na wadogo na wateja wengine wote, ambapo amewakaribisha kuendelea kunufaika na huduma nafuu na rafiki za Benki ya NMB, ambayo ameitaja kuwa benki kubwa kwani ina matawi mijini na Vijiji pia inaongoza kwa kutengeneza faida.

Vilevile ameongeza kuwa, NMB ina huduma zenye manufaa kwa wateja wake ikiwepo mikopo yenye riba  nafuu na Pia Benki hiyo inatoa fursa na kumwezesha Mteja  kujitengenezea faida mpaka kufikia asilimia 12% kupitia huduma ya WEKEZA AKAUNTI ambayo Mteja hulipwa faida ya asilimia 12% ya kiasi Cha fedha  alichowekeza kwa kipindi Cha mwaka mmoja na malipo hufanyika Mara mbili kwa Mwaka.

Pia Mteja Anaruhusiwa kutoa asilimia 20% ya kiasi alichoweka bila masharti na Mteja anapata bima ya Maisha Mara  ajiungapo na huduma hiyo ikiwa ni malipo mara mbili ya kiasi alichowekeza benki.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl. Zainabu Makwinya amesema Halmashauri hiyo itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Benki ya NMB katika Swala zima la maendeleo na utoaji wa huduma Bora kwa umma.

Ikumbukwe, Dunia huadhimisha  Wiki ya Huduma kwa Mteja kila  mwaka katika wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba na kwa Mwaka huu Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni *Nguvu ya Huduma*

Baadhi ya picha za tukio

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi, Richard Ruyango ,Meneja wa NMB tawi la Usa-River Ndg. Mitabalulo Elisha Semuguruka (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya, wakati wauzinduzi wa  Wiki ya huduma kwa wateja tawi la NMB  Usa River.

Picha ya pamoja ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru ,Wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Arumeru ,Meneja na Wafanyakazi wa NMB tawi la Usa River .

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru akizungumza wakati wa maadhimisho ya  Wiki ya huduma kwa wateja katika tawi la NMB Usa River

Wafanyakazi wa NMB wakiwa katika sare maalum wakati wa maadhimisho ya Wiki ya huduma kwa wateja.

Meneja wa NMB tawi la Usa-River Ndg. Mitabalulo Elisha Semuguruka akisoma taarifa ya maadhimisho ya wiki ya Mteja .




Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa