• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WATENDAJI WA KATA WATAKIWA KUSOMA NA KUTEKELEZA ILANI

Imewekwa: September 17th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard  Ruyango, amewataka Watendaji wa Kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru kutatua changamoto na kusimamia miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali katika halmashauri hiyo ikiwa ni kutoa huduma rafiki kwa wananchi.

Mhandisi Ruyango ameagiza  hayo wakati akikabidhi Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha mapinduzi CCM kwa
Watendaji wa Kata 26 za Halmashauri hiyo ambapo amewahimiza kuwa na  mpango kazi  unaolenga utekelezaji wa Ilani ya CCM katika maeneo yao "sisi kama Serikali tunasimamia na Kutekeleza ilani hii iliyopewa ridhaa na wananchi, niwatake mkasome na Kutekeleza ilani hii inayolenga utoaji wa huduma Bora kwa wananchi sambamba na kuwaletea maendeleo" amehimiza Ruyango

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya amesema Halmashauri hiyo imenunua na kugawa ilani kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Watendaji wa Kata Ili kuwawezesha Kutekeleza majukumu yao kikamilifu kwani kwa mujibu wa katiba ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndio inayoiongoza Serikali na Chama hicho ndicho kinacho simamia Serikali" Hamna namna utafanya Kazi nje ya utekelezaji wa Ilani ya CCM hivyo ilani ni nyenzo muhimu izingatieni" amehimiza Mwl. Makwinya

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru  Mhe.Jeremia Kishili  ametoa wito kwa Watendaji na Madiwani kuwa wamoja katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwani Umoja ni msingi wa utendaji bora

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  Watendaji hao wamemshukuru Halmashauri kuwanunulia nyenzo hiyo muhimu na kuahidi kusoma na Kutekeleza ilani hiyo Ili kuharakisha Maendeleo sambamba na utoaji wa huduma Bora kwa Wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango akizungumza na Watendaji wa Kata .

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Akikabidhi Ilani ya CCM kwa Eline Mamuya Mtendaji wa Kata ya Nkoaranga.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru , Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru , Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru pamoja na Watendaji wa Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru.








Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa