• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WATENDAJI WA KATA WATAKIWA KUZINGATIA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI KATIKA MIPANGO YA MAENDELEO

Imewekwa: March 19th, 2018

Watendaji wa Kata kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Meru wamepewa semina  kuwajengea uwezo ili kuzingatia mabadiliko ya tabia ya nchi katika uandaaji wa mipango ya maendeleo jambo litakalo punguza athari zitokanazo na maafa mbalimbali yanayo sababishwa na majanga yatokanayo na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo ndg. Edmund Mabhuye toka Chuo kikuu cha Dar es salaam kituo cha stadi za mabadiliko ya tabia ya nchi  ambaye pia ni mshauri wa mradi wa mfumo wa utoaji wa tahadhari ulio chini ya ofisi ya Waziri mkuu ameeleza kuwa kuna umuhimu wa jamii kupata uwelewa wa kina juu ya mabadiliko ya tabiaa ya nchi kwani  itawawezesha kujiandaa na kukabiliana na madhara ya majanga mbalimbali yatokanayo na mabadaliko ya tabia ya nchi . Nukuu"tutumie  mabadiliko ya tabia ya Nchi kama fursa" amesema Mabuye.

Mtendaji wa Kata ya Majengo ndg. Yohana S. Mollel ameishukuru Serikali kwa juhudi za kuhakikisha wananchi wanapata uelewa wa kutosha juu ya athari za majanga yatokanayo na  mabadiliko ya tabia ya Nchi na kuweza kujiandaa pamoja na kukabiliana nayo kwa kuwajengea uwezo kupitia mafunzo mbali mbali yanayotolewa kwa  wananchii hao na viongoji kuanzia ngazi za chini .

Yohana amesema  Kata ya  Majengo ni miongoni mwa kata zinazoathirika na janga la mafuriko  mara kwa mara yanayosababisha maafa kama vile uharibifu wa makazi ya wananchi pamoja na miundombini  ya barabara hivyo atatumia mafunzo hayo  kuelimisha kamati ya maafa kwenye  Kata yake kuzingatia mabadiliko ya tabiaa ya nchi kwenye mipango ya maendeleo ya mwaka wa fedha 2018/2019  pia amebainisha kutokana na mafunzo mbalimbali yaliyotolewa wananchi wameweza kutumia taarifa za haliya hewa wanazopokea kupitia simu zao za mikononi na kuzitumia "mwezi Februari 2018  wananchi wa kata hiyo walipata taarifa za kuwepo kwa mvua nyingi mwanzoni mwa mwezi Machi 2018 hivyo tume hamasisha wananchi walio kwenye maeneo yanayokubwa na mafuriko kuhama" amesema Yohana.

Mratibu wa maafa kwenye Halmashauri hiyo Digna Masawe amesema kamati ya maafa wilaya imejipanga vyema kuhakikisha kila kata na Vijiji zimeunda kamati za maafa na zinafanya kazi  na kuleta tija kwenye jamii. 

Naye kaimu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Amani Sanga amewataka watendaji hao wa Kata na wataalamu  kutumia mafunzo hayo muhimu katika kutekeleza majukumu yaho.

Picha za tukio.

Ndg. Edmund Mabhuye toka Chuo kikuu cha Dar es salaam kituo cha stadi za mabadiliko ya tabia ya nchi  ambaye pia ni mshauri wa mradi wa mfumo wa utoaji wa tahadhari ulio chini ya ofisi ya waziri mkuu akitoa mafunzo kwa watendaji wa Kata juu ya mabadiliko ya tabia ya nchi.

Miongoni mwa  Watendajin wa Kata wakifuatila mafunzo ya mabadiliko ya tabia ya Nchi yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri.

Miongoni mwa  wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakifuatila mafunzo ya mabadiliko ya tabia ya Nchi yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.

kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Dkt.Amani Sanga akizungumza wakati wa kuhairisha semina ya mabadiliko ya tabia ya Nchi ,kulia kwake ni Mratibu wa maafa kwenye Halmashauri hiyo ndg. Digna Masawe na kushoto kwake ni Ndg. Edmund Mabhuye toka Chuo kikuu cha Dar es salaam kituo cha stadi za mabadiliko ya tabia ya nchi .

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa