• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Watumishi 3 Wilayani Arumeru Wasimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi ya Kilimo cha Bangi.

Imewekwa: July 7th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mheshimiwa Idd Hassan Kimanta amewasimamisha kazi Mtendaji Kijiji na Kata ya Mwandeti,na Afisa Tarafa ya Mukrati kuwa chini ya ungalizi ili kupisha uchuguzi zaidi na hatua kali zitachukuliwa baada ya uchunguzi kukamilika.


Maamuzi hayo yamefanyika katika kikao kazi kati ya Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ,Wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha na Meru, Maafisa Tarafa , Watendaji wa Kata 36  na vijiji 90 pamoja na wakuu wa idara na vitengo katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru.


Aidha Mheshimiwa Kimanta amesema kuna uzembe mkubwa umefanyika katika utendaji wa majukumu yao, hasa kushindwa kudhibiti kilimo cha bangi katika maeneo yao.

“Haingii akilini tokea bangi inalimwa kwa miezi 3 na mwezi wa 4 inavunwa wewe mtendaji wa kata na kijiji upo hapo na hauchukui hatua yoyote”.


Amesema haieleweki kwanini nyie kama viongozi mmeshindwa kudhibiti kilimo cha bangi kwa muda wote huo na mpo hapohapo.


Amewataka watumishi kuacha kufanyakazi kwa mazoea kwani zama hizi niza kuwajibika kila mtu kwenye nafasi yake.


Kimanta amesisitiza zaidi kwa viongozi wa kata na vijiji kuwafichua wote wanaolima bangi katika maeneo yao badala ya kuwaficha,amesema kwa kufanya hivyo wanachangia kuiharibu jamii.


Amewataka viongozi hao wa kata na vijiji kutatua kero za wananchi katika maeneo yao hivyo watakuwa wamewatumika vyema wananchi wao.


Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Arumeru Mkuu wa Wilaya hiyo Mheshimiwa Jerry Muro, amesema tatizo kubwa kwa watumishi wa wilaya hiyo ni kufanya kazi kwa mazoea ndio maana wanashindwa kuchukua hatua mbalimbali za kiutendaji katika maeneo yao.


Aidha, Muro amewataka watumishi wote kuacha kufanya kazi kwa mazoea bali wawe wabunifu zaidi katika kutekeleza majukumu yao badala ya kuwasubiria viongozi wa ngazi ya juu tu.


Mheshimiwa Kimanta amefanya ziara fupi katika wilaya ya Arumeru, baada ya maelekezo yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari John Pombe Magufuli dhidi ya tuhuma za ulimaji bangi katika wilaya hiyo.

Watumishi 3 waliosimamishwa kazi  ni wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mheshimiwa Idd Hassan Kimanta akizungumza wakati wa kikao kazi  na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Wakurugenzi wa Halmashauri 2 za Wilaya hiyo na Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata  26 na Vijiji 90 pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilay ya Meru.

Maafisa Watendaji wa Kata na Vijiji wakati wa kikao na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndg. Jerry Muro  amewataka watumishi wa Wilaya hiyo kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Wakuu wa Idara/Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa kikao na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl. Emmy Mfuru amesema baada ya shule kufunguliwa Walimu wameweka mikakati ya kuhakikisha wanafunzi wanafundishwa sambamba na mihula ya masomo. 

Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Meru ,Mwl. Marcus Nazi amesema Halmashauri hiyo tarehe 4 Julai 2020 iliwapongeza Walimu na Wanafunzi Walioinua Taaluma ambapo Halmashauri hiyo ilifanya vizurii katika mtihani wa Kuhitimu Darasa la saba mwaka 2018 kutoka nafasi ya 40 hadi nafasi ya 23 mwana 2019.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa