• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAZIRI JENISTA AZIAGIZA HALMASHAURI KUWABADILISHIA MIUNDO WATUMISHI,KUWAENDELEZA ILI KUTATUA UPUNGUFU ULIOPO

Imewekwa: October 19th, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama amezitaka Halmashauri za Meru na Arusha  Wilayani  Arumeru kuwabadilishia miundo watumishi sambamba na kutenga bajeti za kuwaendeleza  watumishi waliopo ili kutatua changamoto ya upungufu wa watumishi .

Waziri Mhagama amesema hayo wakati akizungumza na Watumishi wa Halmashauri za Meru na  Arusha Wilayani Arumeru, ambapo amebainisha ubunifu ni muhimu katika kutatua changamoto ya upungufu wa  watumishi waliopo.

Vilevile Mhe.Mhagama amehimiza haki za watumishi kupewa kipaumbele sambamba na kuwa na usawa kwa watumishi katika fursa na uwezeshaji toka Serikalini ili watumishi wajisikie na kujivunia kuwa sehemu katika kujenga nchi hii  "niwatake Wakurugenzi kuhakikisha watumishi wa kada zote wananufaika na fursa   za  Serikali ya awamu ya sita pamoja na kuhakikisha watumishi wanapewa haki zao na kutatuliwa changamoto walizo nazo kwa wakati"amehimiza Mhe.Waziri Mhagama.

Mhe.Mhagama amesema Serikali imewekeza sana kwa watumishi wa umma, ambapo ametoa  wito kwa Watumishi kuweka malengo na kuyatekeleza ambapo amehimiza haki kuenda sambamba na wajibu.

Pia. Mhe.Waziri Mhagama amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya  kwa ujazaji wa taatifa za watumishi kwenye mifumo ambapo Halmashauri hiyo imefika zaidi ya asilimia   96%.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe .John Mongela amesema  mafanikio katika sekta mbalimbali za Mkoa  wa Arusha ni pamoja na mchango wa watumishi, ambapo ameahidi Mkoa kutekeleza maagizo na ma maelekezo yote ya Mhe.Waziri

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya akiwasilisha taarifa ya Watumishi  amesema serikali imeendelea kuboresha maslai ya watumishi katika halmashauri hiyo ambapo kwa kipindi cha mwaka mmoja  imetoa mkopo usio na riba kwa watumishi wa  Halmashauri hiyo kiasi cha Shilingi milioni 600 kuwawezesha kununua vyombo vya usafiri, sambamba na kutoa ajira kwa watumishi 133 wa kada mbali mbali,kupandisha madaraja watumishi 1,245 ambapo amebainisha bado kunaupungufu wa watumishi 696 wa sekta mbali mbali.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa  kuboresha maslai ya watumishi wa kada mbali mbali hivyo kuongeza tija katika kuwahudumia wananchi.

Aidha,Baada ya Kuzungumza na Watumishi Mhe.Waziri anaendelea na ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambapo atatembelea masjala  za ardhi katika Kijiji cha Maweni na Karangai.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na watumishi wa Halmashauri za Meru na Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe .John Mongela akizungumza wakati wa Ziara 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya akiwasilisha taarifa ya Watumishi

Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa ziara ya Mhe.Waziri Mhagama

Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa ziara ya Mhe.Waziri Mhagama


Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa ziara ya Mhe.Waziri Mhagama

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa