• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WITO WATOLEWA KWA JAMII KUSHIRIKI KAMPENI YA UTOAJI WA CHANJO YA POLIO AWAMU YA TATU KUZUIA ULEMAVU WA VIUNGO KWA WATOTO

Imewekwa: August 30th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango ametoa wito kwa wazazi na walezi kushiriki kikamilifu kwenye kampeni ya siku nne ya  awamu ya tatu ya utoaji chanjo ya matone ya  Polio kwa Watoto wenye umri chini ya Miaka 5 (0 -5) ili kuzuia ulemavu wa viungo unaosababishwa na ugonjwa wa Polio.

Akizungumza katika kikao cha uhamasishaji wa chanjo ya polio Halmashauri ya Meru, Mhe.Ruyango amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau imeandaa chanjo na bajeti ya utekelezaji wa  wa awamu ya tatu ya utoaji chanjo ya  matone dhidi ya ugonjwa wa Polio  ili kuhakikisha watoto wote wa Kitanzania  wenye umri chini ya miaka mitano wanakuwa  Salama kwa kupata chanjo hiyo kwani ugonjwa wa Polio umeripotiwa katika nchi  jirani ya Malawi .

Vilevile Mhe. Ruyango ameipongeza Halmashauri ya Meru  kufanya vizuri katika utoaji wa chanjo hiyo awamu ya pili ambapo ilivuka lengo kwa asilimia 138% na kuwataka wataalum kuhakikisha katika awamu hii ya tatu  wanafanya vizuri zaidi kwa  watoto wote  chini ya miaka mitano kupata chanjo ya Polio " nitoe wito kwa wataalam watakao toa chanjo kuhakikisha wanawafikia watoto wote  wenye   umri chini ya miaka mitano " ameagiza Mhe.Ruyango

Mratibu wa chanjo halmashauri ya Meru , Salome Mbegela amesema utoaji  wa chanjo ya Polio awamu ya tatu utafanyika kwa siku nne kuanzia tarehe 01 hadi 04 Septemba 2022 ambapo chanjo hiyo ya matone itatolewa kwa watoto wote wenye umri nchini ya miaka mitano nyumba kwa nyumba  ,vituo vya  kutoa huduma za afya,vituo vya kulelea  watoto , katika shule nk

Dkt.Focus Maneno ambaye ni Mkuu wa Idara ya huduma za Afya, Lishe na ustawi wa jamii amesema chanjo ya Polio ni muhimu sana kwani  ugonjwa wa polio unasababisha mtoto kupooza na kupata ulemavu wa viungo .

Mshili Mkuu wa Meru Ezron Sumari amesema chanjo ya ugonjwa wa Polio ilikuwa toka miaka ya nyuma hivyo ametoa  wito kwa Wananchi wa Meru kutoa ushirikiano katika zoezi la chanjo ya Polio ili watoto wawe salama.

Kwa upande wao Viongozi wa dini waliohudhuria kikao hicho wametoa wito kwa jamii kuhakikisha watoto walengwa wanapata chanjo hiyo muhimu ambapo  Mchungaji Exaud Nnko amesema  ulemavu na kupooza kwa watoto ni janga la jamii nzima hivyo jamii haina budi kuzuia janga hilo kwa kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanapata chanjo.

Aidha, watoto elfu 56,591  wenye umri chini ya miaka 5 wanatarajia kupata chanjo hiyo

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango wakati wa kikao

Mshili Mkuu wa Meru Ezron Sumari wakati wa kikao


Wadau  wakati wa kikao






Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa