• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WITO WATOLEWA KWA VIONGOZI WA DINI, MILA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUHAMASISHA ZOEZI LA SENSA

Imewekwa: August 15th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango ametoa  wito kwa viongozi wa dini, viongozi wa mila, wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji ,Waheshimiwa Madiwani na Watendaji wa Serikali  kuhamasisha jamii kushiriki zoezi la sensa ili Kupata takwimu  za msingi zitakazosaidia kuainisha mahitaji halisi ya wananchi yakiwemo makundi maalum yenye uhitaji maalum kwa mfano, watu wenye ulemavu, wanawake, watoto, vijana na wazee hivyo kurahisisha uandaaji wa sera na mipango ya maendeleo kulingana na uhitaji na mazingira yaliyopo.

Akizungumza kwa nyakati tofauti  na viongozi  wa Tarafa ya Poli na King'ori  Mhe.Ruyango amesema tarehe 23 Agosti 2022 kila Mtanzania aliyelala ndani ya Wilaya hiyo awe Mkazi au la  anapaswa kuhesabiwa  ambapo amehimiza viongozi kuwahamasisha na kuwaelimisha  wananchi kutoa ushirikiano kufanikisha zoezi la sensa ya watu na makazi  " nitoe wito kwenu viongozi mkawe  wazalendo  kwani Tanzania inajengwa na watanzania hivyo tushirikiane kuhakikisha zoezi la sensa linafanikiwa katika maeneo yetu" amehimiza Mhe.Ruyango.

Daudi Wengi  ambani ni Afisa Mipango wa Halmashauri ya wilaya ya Meru akimwakilisha mratibu wa Sensa amefafanua  kuwa  tarehe 23 Agosti 2022 itabaki kuwa tarehe rejea ya Sensa ambapo watu wote waliyolala usiku wa kuamkia tarehe 23 watahesabiwa ambapo ametoa wito kwa wakuu wa  kaya kuwa na taarifa zote muhimu za watu waliolala kwenye kaya yake usiku wa kuamkia tarehe ya sensa ambapo amebainisha taarifa hizo ni umri, jinsi,hali ya ndoa,elimu ,shughuli za kiuchumi ,umiliki wa vitambulisho vya taifa nk

Kwa upande wao Viongozi wa Dini na Mila waliohudhuria  mkutano wa uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi wametoa wito kwa jamii kushiriki zoezi la Sensa ili kutoa taarifa sahihi ili kuwezesha Serikali kutimiza wajibu wake kwa wananchi kulingana na idadi ya watu ya eneo husika " nitoe wito kwa wananchi  kushiriki kuhesabiwa katika zoezi la sensa pia sisi kama viongozi wa mila  hatutaruhusu mtu yeyote kuleta Mgogoro kwenye zoezi la Sensa" amesema Hezron Sumary  Mshili Mkuu Meru

Naye Ramadhan Omary Sheik Wa Usa-River na Amani Halisi Kuhani  wamesema kama viongozi wa dini watahakikisha jamii inaendelea kuhamasika na kushiriki katika zoezi la Sensa kwa maendeleo ya nchi.

Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji pamoja na viongozi wengine wa Halmashauri hiyo wakiongozwa na Mhe.Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki  wametoa wito kwa wananchi kujitokeza kuhesabiwa kwa kutoa taarifa sahihi zitakazotumika kuwaletea maendeleo

Aidha  vikao vya  kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika zoezi la Sensa Vimefanyika katika Tarafa tatu za Halmashauri ya Wilaya ya Meru na kuwa jumuisha  viongozi wa Dini ,Mila ,Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji ,Waheshimiwa Madiwani ,Watendaji wa kata na Vijiji vyote vya Halmashauri ya Wilaya ya Meru .

SENSA KWA MAENDELEO JIANDAE KUHESABIWA


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa