Kata ya Ngarenanyuki,
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya ametoa wito kwa Walimu Kutekeleza wajibu wao Ili uboreshaji wa miundombinu ya elimu iwe na tija katika ujifunzaji na ufundishaji.
Mwl.Makwinya ametoa wito huo alipotembelea Shule ya Sekondari ya Momela kukagua vyumba 4 vya Madarasa ambavyo vimejengwa kwa michango ya Wananchi, wahisani na Halmashauri ilichangia mbao na bati, Mradi wa vyumba 2 vya Madarasa ya EP4R pamoja na ujenzi wa chumba kimoja Cha darasa kwa nguvu za kikundi Cha kimila.
Mwl.Makwinya amesema ni muhimu kwa Walimu kuitendea haki michango ya Serikali na Nguvu za Wananchi kwa kuwajibika kwa weledi ili mtoto wa kitanzania aweze kupata Elimu itakayo mnufaisha.
Diwani wa Kata ya Ngarenanyuki Mhe.Aminiel Mungure ameishukuru Halmashauri kwa kutoa bati na mbao na kuomba kukamilisha nyumba ya mwalimu.
Vilevile .Mhe.Mungure amewapongeza Walimu kwani kwa sasa Shule hiyo inafanya vizuri kitaaluma.
Aidha, Kata ya Ngarenanyuki ni Miongoni mwa Kata saba ambazo Mkurugenzi Zainabu amefanya ziara ya kukagua na kutembelea utekelezaji wa miradi ya EP4R ,Miradi ya Nguvu za wananchi na michango ya wahisani,miradi ya TASAF pamoja na maboma ya muda mrefu ,ambapo aliambatana na Afisa Elimu Sekondari pamoja na Waandisi wa Ujenzi toka Halmashauri.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya akiwasili Shule ya Sekondari Momela Kata ya Ngarenanyiki.
Picha ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya (wa tatu kutoka kushoto) na Diwani wa Kata ya Ngarenanyuki .Aminiel Mungure pamoja (kulia), viongozi,Walimu na Wanachi wakati wa ukaguzi wa vyumba 4 vya Madarasa
Ujenzi wa vyumba Viwili (2)vya Madarasa ya EP4R katika Shule ya Sekondari Momela
Maabara katika Shule ya Sekondari Momela
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa