Umoja wa wanawake wa Meru wamempongeza Mhe.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwaamini Wanawake na kuendelea kuwateua katika nyadhifa mbali mbali.
Mwenyekiti wa Umoja huo Bi.Furahisha Magubila akizungumza kwa niaba ya Wanawake wa Umoja huo ,wakati wa hafla ya kumkaribisha na kumpongeza Mkurugenzi mpya wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, amemshukuru na kumpongeza Mhe.Rais kwa Kumteua Mwl.Zainabu Juma Makwinya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, kwani tangu kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo haijawahi kuongozwa na Mkurugenzi Mwanamke.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya amemshukuru Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kwenda Meru kushirikiana na wanameru ili kusogeza Halmashauri hiyo mbele katika Swala zima la maendeleo.
Aidha. Mwl. Makwinya amewaomba ushirikiano wanameru huku akiwahakikishia wanawake kuwa asilimia kumi ya mikopo itawafikia kwa wakati ambapo amewataka kuwa Chachu ya kuhimiza wakina mama kujitokeza kujiunga kwenye vikundi kwa ajili ya mikopo hiyo itakayo wasaidia kujikwamua kiuchumi.
Akihitimisha Mwl. Makwinya amewashukuru Wanawake kwa upendo huo na kuhimiza ushirikiano kwa Serikali kuwa endelevu sambamba na kila mwanamke kuwa jicho kwenye mapato ya Halmashauri kwa kuhimiza jamii kulipa tozo za Halmashauri kwa maendeleo"mapato yakiongezeka na asilimia Kumi inaongezeka,tulipe tozo kwa maendeleo yetu"amehimiza Makwinya.
Nao Wanawake wanasiasa wa Meru akiwemo mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) Wilaya ya kichama ya Meru, Julieth Maturo na makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Felister Nanyaro wameahidi kumpa ushirikiano Mkurugenzi Zainabu na kumkaribisha Meru"Wanawake ni jeshi kubwa, hatuna budi kushirikiana kwa kuwaunga Mkono Viongozi Wenzetu" wamesema wanasiasa hao.
Ikumbukwe Halmashauri ya Wilaya ya Meru ilianzishwa Mwaka 2007.
Wanawake wa Umoja wa Wanawake Meru wakimpongeza Mwl.Zainabu Makwinya
Wanawake wa umoja wa Wanawake Meru wakimlaki Mwl.Zainabu Makwinya (wa kwanza)alipowasili eneo la tukio.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya (katikati),Mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) Wilaya ya kichama ya Meru ,Julieth Maturo (kulia) na Makam Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Felista Nanyaro wakikata Keki ya ukaribisho .
Mwl.Zainabu Makwinya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Meru akizungumza na Wanawake wa Meru
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa