Wajumbe wa kamati ya utawala, fedha na mipango wakiongozwa na mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili wamefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa kipindi cha robo ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2023/2024.
Aidha, katika ziara hiyo wananchi wa kata zilizotembelewa wametuma Salamu kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za maendeleo kwenye maeneo yao "tunashukuru Kata yetu ya Kikatiti tumepokea Miradi mingi ,zahanati imekamilika,nyumba ya mtumishi imekarabatiwa, uboreshaji sekta ya Elimu tumenufaika na leo tunafuraha Madiwani mnakagua ujenzi wa Uzio kwenye soko letu la kikatiti "Amesema Nuru Mkazi wa Kikatiti
Ikumbukwe Baraza la Halmashauri linaongozwa na Mhe.Kishili linaweka historia kuwapelekea wananchi wa Pembezoni maendeleo ambapo limetoa shilingi Milioni 400 za mapato yake ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Maroroni
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa