Msimaamizi wa uchaguzi Halmashauri ya Meru , Jonathani Kiama amesema zoezi la kuchukua na kurejesha Fomu za wagombea wa nafasi ya uenyekiti wa Kijiji, ujumbe wa Halmashauri ya Kijiji kundi mchanganyiko, Ujumbe wa Halmasshauri ya kijiji kundi la wanawake na unyekiti wa Kitongoji katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru na Mamlaka ya Mji mdogo wa Usa- River limeenda vizuri ambapo wagombea wa Vyama mbalimbali wameweza kuchukua na kurejesha fomu.
Aidha Kiama amesema katika zoezi hilo kumekuwa na changamoto kutoka kwa baadhi ya Viongozi wa Vyama vya siasa kutoa taarifa za upotoshaji kuhusiana na zoezi zima la kuchukua na kurejesha fomu ,mfano taarifa zilizotolewa zikieleza kuwa, Wasimamizi wasaidizi katika Vijiji vya Sura na Kilinga vilivyopo Kata ya Songoro kutokwepo Ofisini jambo ambalo si kweli kwani alipofika katika vijiji hivyo aliwakuta wasimamizi wasaidizi wakiendelea na zoezi la kutoa na kurejesha fomu za ugombe kwa Vyama mbalimbali .
Kiama ameeleza kuwa baada ya zoezi la kuchukua na kurejessha fomu za ugombea kukamilika leo tarehe 04 Novemba 2019 Saa 10:00 kamili jioni , zoezi linalofuata ni zoezi la uteuzi wa wagombea wa nafasi ya Uenyekiti wa Kijiji, Ujumbe wa Halmashauri ya kijiji kundi mchanganyiko, ujumbe wa Halmashauri ya kijiji kundi la Wanawake,Unyekiti wa Kitongoji
Zoezi la uteuzi litafanyika Kesho tarehe 05 Novemba 2019 , hii ni kwa mujibu mujibu wa jedwali la matukio ya uchaguzi lillilotolewa katika Muongozo wa uchaguzi wa viongozi wa ngazi za Vijiji, Vitongoji na Mitaa utakao fanyika terehe 24 Novemba 2019.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa