• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC ARUMERU- TUWAUNGE MKONO VIJANA WAJASIRIAMALI

Imewekwa: August 20th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Kaganda amewataka wananchi na wakazi wa Meru kuunga mkono juhudi za vijana wajasiriamali wadogo wadogo ili kuweza kuwainua kiuchumi.

Ametoa wasaa huo mapema Leo katika tamasha la maadhimisho ya siku ya Vijana duniani yaliyoadhimishwa Kata Usariver viwanja vya Ngarasero katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

"Niwaombe sana watanzania wenzangu na Wana Arumeru tuwaunge mkono vijana wanaotengeneza bidhaa za asili na bidhaa nyingine zinazotengenezwa katika Wilaya yetu ili vijana watoke kwenye kundi la wajasiriamali wadogowadogo na mwisho wa siku waanzishe kiwanda ambacho kitaweza kuajiri vijana wengi zaidi" Amesema Mhe. Kaganda.

Aidha, Mhe. Kaganda ambaye amekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, ameipongeza Halmashauri kwa kutoa Pikipiki 40 kwa Vikundi vya vijana kupitia mikopo ya asilimia 4% kutoka Halmashauri ya Meru na kufanya marejesho yao vizuri kama inavyotakiwa.

"Niwapongeze sana Halmashauri ya Meru Kwa kutoa pikipiki zaidi ya 30 Kwa Vikundi vya usafiri wa bodaboda kwani nimesikia wanafanya vizuri sana katika marejesho na ningependa kuonana nao kwani sekta ya usafirishaji ni sekta muhimu sana " Amesema Mhe. Kaganda.

Maadhimisho ya siku ya Vijana Duniani yalianzishwa na Umoja wa Mataifa (UN) mwaka 1999 Kwa kupitishwa na Azimio 54/120(1) Kwa lengo la kuhamasisha masuala ya kiutamaduni na kisheria yanayowahusu vijana.

Hata hivyo, Halmashauri ya Wilaya ya Meru Kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa mashirika yasiyo ya kiserikali imeadhinisha siku ya vijana Duniani Leo tarehe 20.08.2023 iliyoambatana na michezo mbalimbali kama vile Mashindano ya kukimbia Km 10 na Km 5, maonesho ya vikundi vya wajasiliamali, kukimbia na gunia, kuvuta kamba, burudani pamoja na uchangiaji wa damu salama na kupima Afya.

Kauli Mbiu 2023:"KIJANA CHAPA KAZI BILA KUATHIRI MAZINGIRA"

Picha na matukio bofya https://merudc.go.tz/single-gallery/matukio-maadhimisho-ya-siku-ya-vijana-duniani-20082023


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa